Posts

Showing posts from August, 2016

Chocolate Zinavyohusishwa na ‘Uwezo wa Akili’ Kwa Wanafunzi Darasani

Image
Wakati wazazi wengi nchini wakihaha kudhibiti ulaji holela wa vitu vitamu kwa watoto wao ili kuimarisha afya ya kinywa. utafiti mpya wa hivi karibuni umeibuia mapya baada ya kubainika kuwa ulaji mzuri wa chocolate unaweza kuongeza uwezo wa kufikiri na hivyo kutoa fursa kwa watoto kufanya vizuri darasani. Aidha, utafiti huo umebaini vilevile kuwa ulaji wa chocolate husaidia kupunguza kasi ya kawaida ya kuzeeka kwa walaji itokanayo na kuongezeka kwa umri. Ripoti ya utafiti huo ilitolewa hivi karibuni, inabebwa na utambulisho usemao ‘ulaji wa chocolate huongeza utendaji kazi wa ubongo” na kwamba ”unaweza kusaidia mtu kutozeeka haraka licha ya umri kuzid kumtupa mkono’ Utafiti huo uliochapichwa mwezi huu katika jarida la Appetite, umebaini kuwa kumbukumbu na uwezo wa kufikiria ufumbuzi wa mambo magumu kuwa katika kiwango cha juu kwa watu wanaokula chocolate kwa wingi. Matokeo hayo yameripotiwa kutoathiriwa na umri wa mlaji, uzito wa mwili wala aina nyingine za ulinganifu wa

Mwimbaji Ruby Akimbilia EFM Radio Baada ya Ugomvi wa Maslahi Kati ya Mwimbaji Huyo na Clouds FM

Image
Pichani Ruby akiwa Kwenye Tamasha la EFM Mwimbaji Ruby ambae alikuzwa na kulelewa na Clouds FM Baada ya Kufanya vizuri katika mashindano ya Fiesta Diva Nyota miaka kadhaa iliyopita amejikuta katika ugomvi wa kimaslahi na walezi wake Clouds FM baada ya kushindwana malipo katika Matamsha ya Fiesta yanayoendelea hivi sasa.. Ruby kwa sasa inaonekana amekimbili kwa washindani wa Clouds FM ambani ni EFM Radio, Radio hiyo mpya ambayo ni washindani wa Clouds FM kwa jijini Dar es Salaam wamechukua fursa hiyo na sasa wanamtumia katika matamasha yao ya Mziki Mnene Sehemu mbali mbali... Je unaona ni sahihi Ruby Kufanya hivyo?

PICHA: Diamond Avunja Rekodi Meru, Kenya

Image
Diamond Platnumz ana miaka mingi ya kuvuna mapesa kutokana na show zake. Kutoka kwenye mapokezi yaliyovunja rekodi, Meru nchini Kenya hadi kuangusha show iliyohudhuriwa na makumi kwa maelfu ya mashabiki wenye kiu, staa huyo ameendelea kujiweka kwenye ligi yake mwenyewe.  Ilikuwa ni show ya mtu mmoja na kwa picha alizoweka kwenye page yake ya Instagram, inaonesha jamaa alihama na kijiji. Tazama picha hapo chini.

Shamsa Ford kufunga ndoa Ijumaa hii

Image
Msanii wa filamu Shamsa Ford anatarajia kufunga ndoa Ijumaa hii na mfanyabiashara wa nguo aitwae ‘Chidi Mapenzi’. Shamsa na Chidi Mapenzi Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa ndoa hiyo itafanyika nyumbani kwa wazazi wake Sinza Africana jijini Dar es Salaam. “Kweli bhana Ijumaa hii Mungu akipenda nafunga ndoa,” alisema Shamsa Ford. Miezi mitatu iliyopita mfanyabiashara huyo alikiri kuwa kwenye mahusiano na malkia huyo wa filamu na kuweka wazi mpango ya ndoa.