Posts

Showing posts from September, 2016

HEKAHEKA: Ajifungia ndani na kujichoma kisu, majirani waelezea kilichopelekea ajiue

Image
September 27 2016 kupitia Hekahek a ya Clouds FM Geah Habib  amekutana na hii iliyotokea Tandale jijini Dar es salaam ambapo mwanaume mmoja amejiua kwa kujichoma kisu, majirani waeleza ni baada ya kugundulika kuwa ameathirika na virusi vya UKIMWI,  millardayo.com imekurekodia full stori kutoka kwenye Hekaheka ya leo. >>>’Alikuwa anaumwa TB alikuwa anatumia dawa na mimi nilikuwa nimekaa naye majira ya saa 12 akaniagiza vocha, narudi nakuta mlango umefungwa, nikampiugia simu ikwa inaita tu hapokei’:- Mke >>> ‘Tulianza kuchungulia dirishani naona mlango kwa ndani umefungwa, majirani wakachungulia wakaona mtu kalala, ikabidi wanisaidie kuvunja mlango kufungua tukakuta kisu kipo shingoni’;- Mke ‘walivyoenda akapima akaonekana ana virusi akamwambia mkewe kuwa mimi mgonjwa, na leo asubuhi alidondoka ndio akajua hii safari kwa sababu hivi virusi kwanini vimefikia hivi na vimeniamaliza haraka, watu wak

Mabasi ya Haraka yalivyogongana yenyewe kwa yenyewe DSM

Image
Ikiwa ni siku kadhaa zimepita tangu UDART kujenga control room katika kituo chao cha Jangwani ambapo imekuwa na msaada wa kumonitor madereva. Leo September 26 2016 eneo la Magomeni Usalama jijini Dar es salaam kumetokea ajali iliyohusisha mabasi mawili yaendayo haraka baada ya kugongana yakiwa kwenye njia yake. Abiria wote walitoka salama na hakuna madhara yoyote kwa abiria.

INSTAGRAM: Maneno 205 aliyoyandika Ray C kwa Diamond Platnumz

Image
Mrembo kutoka bongoflevani Ray C leo September 27 2016  amezichukua headlines kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya kumuandikia ujumbe wa salamu wenye maneno 205 hitmaker wa mdundo wa ‘ Salome’ Diamond Platnumz , Mtu wangu ni kazi yangu kukuletea stori zote ambazo zinachukua headline kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii. Haya ndio maneno kwa Ray C kwa Diamond Platnumz.. >> ‘ Seriously Namaste lil bhaia!ngoja niwe mkweli wa nafsi yangu nipate nafuu dude!that Salome of Yours is damn hot!The Powerful couple in this industry kwa sasa bila ubishi wangu ni hawa wachapakazi wawili,bidii katika kila walifanyalo,go getters,wanavyopeana nguvu katika kazi zao,team work team work team makes everything go the it should be and that makes me fall in love with these two hard working souls!everysecond of the day,lil bro u really smart dude,i respect you for that roho ya upendo ulionayo ndio inayozaa matu

Wanaume Siku Hizi Mbona Mnalia lia Sana Kuchunwa?

Image
Hata maandiko matakatifu yameandikwa mwanaume utahangaika juani ili umlishe mkeo na mwanamke atazaa kwa uchungu, sasa imekua siku hizi wanaume kumhudumia mwanamke imekua ni kulia lia sana mwanaume wa ukweli anatakiwa ajue mpenzi wake au mke anamhudumia vipi. Hivi mnadhani nyie wavulana unakua hujaoa una mpenzi tu unataka aishi vipi unakuta unatoa vielfu 50 unalalamkika mpaka povu linakutoka unataka kumiliki msichana mrembo mzuri huku unatoa kihamsini unalalamika sana starehe gharama ukiona vyapendeza ujue vimegharamiwa. Ebu kueni wastaarabu basi kutwa kulia lia humu JF, mnawadhalilisha sana kina dada anakuja kwako kajigharamia mwenyewe mapouda nini unamgaragaza unamtindua wewe ukimpa kihamsini unalalamikaaaaaa sasa unatakaje? Acheni hizo basi ukimtoa out akija na rafiki yake wakinywa savana tu mnalia sasa mnataka wanywe viroba? Au safari?

Tuzo nyingine kubwa ambayo Alikiba amechaguliwa kuwania

Image
Majina ya washiriki katika  tuzo kubwa mbalimbali yamekua yakiendelea kutajwa na tuzo nyingine ambayo majina ya wanaowania  yametajwa ni tuzo za MTVEMA, ambazo  Alikiba ametajwa kuwania kama msanii bora kutoka Afrika. Tuzo za ( MTVEMA ) MTV Europe Music Awards  ni tuzo za mziki za MTV barani Ulaya ,kama ilivyo MTVMAMA kwa Africa.  Kupitia mtandao wake wa Instagram Alikiba ameeleza jinsi ambavyo mashabiki wake wanaweza kumpigia kura.

Jinsi ya Kumlinda Mumeo Asichepuke

Image
Wanawake wengi hawajui nafasi ya mume, hivyo kufanya mambo kiholela na kujikuta NDOA inaanza kuleta matatzo. Jinsi ya kumlinda mumeo: 1. MAPISHI Unapokua upo jikoni unaandaa chakula, ni lazima ujue kuwa anaekula ni mumeo, hivyo ni vizuri ukatumia ujuzi wako wote kuhakikisha mumeo anakula chakula kizuri. Wanawake wanapika chakula kizuri siku za sikukuu ndo anajitahidi kutumia uelewa wake wote katika kupika ili tu aonekane na majirani. Au siku ukisikia mumeo anakuja na mgeni rafki yake alafu yamkini ni mtu mwenye cheo fulani ndo unataka upike vizuri. KWA IYO USITAKE KUPIKA VIZURI ETI KWA SABABU KUNA MGENI AMEKUTEMBELEA BALI IWE NDO TABIA YAKO KWA MUMEO 2. USAFI Wanawake bado hawajajua kuwa usafi ni kivutio pia kikubwa kwa mwanamume. Na kama tunavyojua kuwa usafi maana yake ni "kila kitu mahali pake" Sasa wanawake utakuta vijiko vya chakula vipo kwenye kitanda eti kwa sababu tu ana mtoto mdogo. Au nguo za mikojo ya mtoto unaweka chini ya kitanda m

Kupatwa Kwa Mrembo Huddah: Azama Kimapenzi Kwa Mchagga!

Image
Haya jamani yule Sosholaiti wa Kenya kazama kwa Mchaga wa Kishumundu (Sina uhakika). Kaka huyo ajulikanaye kama Danford Kessy amemteka mrembo huyo ambaye amekiri kuwa ni muda mrefu amekuwa akijilinda lakini sasa amefika bei kwa Mkaka huyo Handsome Tazama Picha ya mwanaume huyo hapa:

Salam za Mama Diamond Platnumz kwa Wema Sepetu

Image
September 28, 2016 ni siku ambayo anazaliwa mrembo na mwigizaji wa Filamu, Wema Sepetu ambapo pamoja na watu wengi kumtakia kila la kheri  yupo pia Mama mzazi wa Diamond Platnumz ambaye kwenye akaunti yake ya Instagram amepost picha ya Mama yake Diamond akaisindikizia na maneno haya .. >>> H appy birthday.. Mamy akee @wemasepetu mungu akuongezee umri na akujali kheri akufungulie Mlango wa baraka kwa kila uliombalo.Amin

Agness Masogange Aamua Kupima Ukimwi na Kutuonyesha Kukata Mzizi wa Fitina

Image
Baada ya Mrembo Tunda kuanika Majibu yake ya Ngoma tukayaona...Agnes Masogange nayeye awafunga midomo walikuwa wakimsema ana Ugonjwa...Aanika wazi majibu yake. .imethibishwa kuwa Hana HIV...je ukipata nafasi utamshauri nini? ?? Tia neno kwako

Taarifa za uzushi kuhusu kifo cha muigizaji Muhogo Mchungu.

Image
Kumeibuka  taarifa zisizo sahihi ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii haswa Whatsapp na Instagram kuhusiana na muigizaji mkongwe wa filamu Tanzania, Muhogo Mchungu kufariki dunia. Baada ya taarifa hizo kuenea, kupitia mtandao wake wa Instagram, mwigizaji wa bongomovie Batuli amekanusha taarifa hizo. Batuli aliandika hivi… ” Muogopeni Mungu Nyie Mnaozusha Habari Za Vifo Kwa Watu Maarufu,, Mkumbuke Hakuna Atakayepaa Sote Njia Yetu Ni Moja, Tumieni Mitandao Vizuri Sio Sifa Wala Ujanja Kutengeneza Habari Zenye Uzushi Kila Baada Ya Muda Fulani, Kifo Ni Cha Wote Hakikimbiliki Mtambue Ipo Siku Na Nyie Mabingwa Wa Kuzusha Kitawatembelea Tu #MunguAnawaona #MolaAkupeMaishaMarefuBaba ”

Chidi alikuwa apelekwe Ulaya kwenye matibabu kama angemaliza muda wa matibabu Sober House – Kalapina

Image
Rapper Kalapina mmoja kati ya wadau ambao walimsaidia Chidi Benz kumpeleka Sober House amefunguka kwa kusema kuwa kitendo cha Chidi Benz kukatisha muda wa matibabu akiwa Sober House kumemkosesha vitu vingi pamoja na kupelekwa Ulaya kwa ajili ya matibabu. Akiongea katika kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio Jumanne hii, Kalapina amesema Chid Benz alikuwa hajapata matibabu sahihi alipotoka ‘sober house’. “Chid Benz hakumaliza muda wa matibabu alivyotoka ‘sober house’ ndani ya siku 28, kwahiyo mi namuomba afikirie faida alizozipata sober na faida anazozipata sasa hivi akiwa mtaani, nafasi bado ipo kwake kwa sababu tumeplay part kubwa hadi Chid Benz akae sawa, kwa hiyo anatakiwa atusikilize, nafasi ipo kubwa kwa Chid Benz kuweza kujisahihisha”, alisema Kalapina. Kalapina amesema Chidi Benz alipata wafadhili wa kumpeleka nchi za nje kwa matibabu zaidi, lakini ikashindikana kutokana na kitendo hicho. “Kulikuwa kuna safari ya yeye na Ray C kupelekwa Ulaya, wa

Mwanamuziki Trey Songz na Vanessa Mdee Mambo Safi..Trey Asema Haya

Image
Trey Songz amefunguka kuhusu kufanya kazi na Vanessa Mdee wakati akijibu swali la shabiki. Wakati akijibu swali hilo muimbaji huyo wa Marekani amesema wametengeneza wimbo mzuri pamoja. “Vanessa is great, we got a great song together, has a great chemistry, she loves to laugh and joke even when we was performing having a good time,” alisema. Kuna uwezekano mkubwa Vanessa na Trey Songz wakaka kutengeneza wimbo wa pamoja nje ya Coke Studio.

Atumia Asali Kufanya Sehemu Nyeti Kuwa Ndogo na Kubana, Nyeti Zaoza

Image
Nawaletea Kama Nilivyotumiwa: Miaka 3 iliopita nimekuwa katika matatizo makubwa sana nawashwa sana ukeni, hospitali wanasema ni fungus, natumia dawa baada ya wiki tatizo linarudi pale pale, nimekuwa mtu wa kujikuna muda wote, uchi unawaka moto kwa kujikuna, nimeendelea na tiba mpaka likaibuka tatizo lingine. Kila ninapofanya tendo ndoa napata maumivu ambayo hayaelezeki wakati mwingine mpaka naanza kubleed, kurudi tena hospitali wakasema nipime vipimo vya kansa, ikabidi watoe kinyama ndani na kufanya vipimo, majibu yalipotoka wakasema hakuna kansa lakini tatizo linazidi kuongezeka siwezi tena kufanya tendo la ndoa lakini madaktari katika vipimo vyao wakagundua ndani ya uke kwenye mlango wa kizazi kuna wekundu mwingi sana, badala ya rangi ya pink kumbe ile rangi nyekundu ni sehemu ambayo inashambuliwa sana na bacterial wasiosikia dawa, wakajaribu kupeleka dawa hapo kwenye hilo eneo lililoathirika bado ilishindikana kuwaua walikuwa bado wanaonekana wanasham

Kama Wewe Mwanaume Una Tatizo la Kufika Kileleni Haraka Kabla Mpenzi Wako Hajaridhika Hii Inakuhusu

Image
Pre mature ejaculation ni nini? Hii ni hali ambayo mwanaume anatoa mbegu mapema sana kipindi cha tendo la ndoa na mara nyingi huambatana na kushindwa kumridhisha mpenzi wake. Tatizo hili limekua likiwapata wanaume wengi na kujisikia aibu mbele za wenzi wao pale wanaposhindwa kuendelea kabisa baada  ya hali hii kutokea. Kimsingi  mwanaume anatakiwa achukue dakika nne mpaka nane kabla ya kutoa mbegu za kwanza lakini watafiti wanasema tatizo hili hugundukiwa mtu anapotoa mbegu ndani ya dakika moja au kabla ya dakika moja. Tatizo hili huweza kutokea mara tu baada ya kubalehe,{primary pre mature ejaculation} mda mrefu baada ya kubalehe{secondary PE} au kutokana na aina ya mwanamke uliompata.{situational PE} Chanzo ni nini? Tatizo hili halina sababu za kitaalamu zilizofanyiwa utafiti zikakakubalika ila wanasayansi wanaamini sababu zifuatazo zinaweza kua chanzo kikuu cha tatizo hilo. Kupiga punyeto au kujichua;  mara nyingi watu wanaopiga punyeto hua wanafa

Ushahidi Huu Hapa Mungu Amekataza Mapenzi Kinyume na Maumbile

Image
Kitabu cha Biblia kinaeleza waziwazi huu uchafu unaofanywa na binadamu kama matendo ya ushoga,kutembea na binamu yako pamoja na wake za watu,kupitia vifungu vifuatavyo : USHOGA NA ULAJI TIGO MAMBO YA WALAWI 20:13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume,kama alalavyo na mtu mke,wote wamefanya machukizo hakika watauwawa KUTEMBEA NA MKE/MUME WA MTU MAMBO YA WALAWI 20:10 Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine,na mwanamke aziniye na mtu mume hakika watauwawa NA WALE MNAOKULA KUKU NA MAYAI YAKE [MAMA NA MWANA] MAMBO YA WALAWI 20:12 Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauwawa,Tena mtu mume akimuoa mke pamoja na mama yake ni uovu mkuu WALE WANAOTEMBEA NA WANYAMA MAMBO YA WALAWI 20:15 Tena mtu mume akilala na mnyama, na mwanamke akimkaribia mnyama yeyote na kulala pamoja naye,mtamwua huyo mwanamke KUTEMBEA NA BINAMU YAKO MAMBO YA WALAWI 20:19 Usifunue utupu wa umbu la mama yako wala umbu la baba yako Tunakumbushana tuu Jamani

Utata wa Nyumba Mpya ya Diamond Waibuka

Image
Habari zilizo chini ya carpet huku Instagram ni kuhusu nyumba mpya ya mwanamuziki Diamond iliyopo South Africa zinasema kuwa mjengo huo bado haujalipiwa na uko sokoni kama picha inavyoonyesha hapo. Hivyo si Diamond wala Zari wana umiliki halali wa hiyo nyumba...... Mdaku Mmoja Huku Instagram Ameandika yafuatayo: Tzshaderoom "#roommates nilipost since angalieni post za nyuma nilikuwa wazi. Inasemekana #zari alikuwa akimkosesha Amani #chibu anunue nyumba south coz #ivan hamtaki mwanae kwake. Then msg zilizokuwa zinaeleza #zari atoke ktk nyumba #ivand akazisambaza kisa #mondi kapost nyumba akidai kuwa kamnunulia zari 😂 guys nilikwisha Sema kigoma hapatoki fala uzalendo Kwanzaa 🙌 do you think if #mondi hakuwadhibiti na Ile post yoote yanayo jiri tungeliyajua 🤔 jibu unalo. #zari na #ivan ni business partners now naomba nifunguke. Zari came in Tz kwa Nia ya kufanya kazi na #mondi akawazunguka walio kuwa wanandaa kazi hiyo ifanyike akaomba no. za mondi

Madhara ya Kutofanya Tendo la Ndoa Muda Mrefu

Image
Habari zenu, nimeona niwaletee hili nina imani mtajifunza hasa kwa wale wasiofahamu,Ukikaa Muda Mrefu bila Kufanya tendo la Ndoa madhara yake ni kama haya: Hasira za mara kwa mara katika mambo madogo, kupendelea sana kuangalia picha za uchi, Kusahausahau, Kupendelea story za mapenzi, Kutokwa damu nyingi wakati wa hedhi (Mke), Kupenda kurukiarukia mambo ya watu wengine (tabia ya kufuatilia mambo yasiyokuhusu), Kuumwa na kichwa, Kukakamaa mgongo (wanaume), Kuingiliwa kirahisi na jini mahaba, Kupoteza umakini ktk kazi (efficiency), Siku ukikutana kimwili na mwenye virusi bila kinga utaambukizwa kirahisi mno, Waweza ku-develop tabia mpya ambayo hukuwahi kuwa nayo ili iwe mbadala kama ulevi n.k.

Dongo la Diamond Lamtoa Mapovu Aliyekuwa Mume wa Zari Ivan....Meseji zavuja Zari Akimuomba Msamaaa

Image
Hali ni Tete Madale....Dongo la Diamond aliloandika kuhusu wale wanaojisifu kuwa wanahela lakini watoto wao wanaishi kwenye nyumba ya kupanga limemfikia mwenyewe ambae ni mume wa dhamani wa Zari aitwaje Ivan , Nimepitia kwenye mitandao nimekuta mazungumzo yaliyovuja ambayo yanasemekana ni kati ya Zari na Ex Wake huyo baada ya Ujumbe wa Diamond Kuwafikia mpaka watoto wao ambao walizaa pamoja. Nimekuwekea Hapa hayo mazungumzo ambayo yasemekana yamevuja kutoka kwa mmoja wao:

Baada ya Kusimangwa Mtandaoni Kuwa Anafanya Umalaya Mrembo Tunda Apima Ukimwi na Kuonesha Majibu Hadharani

Image
Mrembo wa Nguvu na Mcheza Video Tunda amechukua maamuzi magumu ya kwenda kupima ngoma na kutundika majibu yake mtandaoni baada ya baadhi ya wadau hasa kutoka Instagram kumsema kuwa anafanya umalaya kutokana na muda wote kupiga picha akiwa kwenye mahoteli makubwa akila bata za nguvu na hana kazi maalum ya kufanya mjini hapa..... Nimekuwekea majibu yake hapa chini:

Sababu Kubwa Ambazo Zinamfanya Mwanamuziki Diamond Aendelee Kufanikiwa Zaidi na Zaidi na Kuwapita Wenzake Hizi Hapo

Image
Unadhani kwanini pamoja na kuwa kinywaji na brand maarufu duniani, Coca-Cola inaendelea kumwaga fedha nyingi kwaajili ya matangazo? Kampuni hiyo hutumia zaidi ya dola bilioni 3 duniani kote kwaajili ya matangazo kila mwaka. Kwanini sasa wanahitaji fedha nyingi kiasi hicho kujitangaza wakati kila mmoja katika dunia hii anaijua Coca-Cola? Ni hivi – matangazo hayakukumbushi uende kununua soda pale unapokuwa na kiu – lahashaa! Kazi yake ni kuhakikisha jina lake linakaa zaidi kichwani kwako, na ni jina ndilo unalolinunua. Kwahiyo watahakikisha wanajitangaza ili ile nembo ya Coca-Cola ikae daima kichwani kwako. Mfano huu unahusiana vipi na Diamond? Kwa ukubwa wote alionao, mashabiki wote hao alionao, kwanini bado anaendelea kuzipigia promo ngoma zake kiasi hicho? Kwa hatua aliyofikia, anaweza kuachia wimbo na kutoa link mara moja tu na mashabiki wenyewe wakashughulika nao, lakini hafanyi hivyo. Akitoa wimbo ataupigia promo kwa kuweka post kibao kila siku. Pro

Familia ya Diamond Yaikacha Sherehe ya Birthday ya Zari Iliyofanyika Zanzibar...Mabifu Yaibuka Upya

Image
MWISHONI mwa wiki iliyopita (juzi Ijumaa usiku) ilifanyika pati ya kusherehekea kuzaliwa kwa mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari’ ambayo imeibua mabifu upya. Pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa wachache kutoka Bongo ambao ni pamoja na Moze Iyobo, Aunt Ezekiel na wengineo ilifanyika Zanzibar ambapo licha ya kufana, imeibua mtifuano upya kati ya Zari na wifi yake, Esma Abdulkadiri na Diamond na mume wa zamani wa Zari, Ivan Semwanga. IVAN NA DIAMOND Bifu la wawili hawa lilikuwa limezimika, lakini lilirudi upya baada ya juzikati Diamond kumzawadia Zari nyumba iliyopo Afrika Kusini kisha kumrushia Ivan dongo kwa kuandika mtandaoni: “Wanakazana kujisifu matajiri ilhali watoto wao wanaishi kwenye nyumba za kupanga… halafu leo yuleyule wanayemtukana kutwa kwenye mitandao kuwa maskini, kajawa na shida, kanunua nyumba kulekule kwao ili watoto wao waishi maisha bora kama wanayoyatamani… Heri ya siku ya kuzaliwa Mama tee wangu…. N

Pamoja na Drama Zote Alizompa Sugu...FAIZA Ally Anampenda Mbunge Sugu Kupindukia...Soma Alichoandika Hapa

Image
Msanii wa filamu, Faiza Ally wakati inaelekea siku ya birthday ya mtoto wake Sasha, amefunguka na kueleza yamoyoni juu ya baba watoto wake, Mh Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Sugu na Faiza Mwigizaji huyo ambaye anajipanga kuachia filamu yake mpya ‘Baby Mama Drama’ amesema ataendelea kumpenda Mh Sugu kwa kuwa bila yeye asingekuwa mama kwa sasa. “Nakumbuka 2012 wakati kama huu nilianza kuumwa uchungu wako mwanangu. Yaani nilikua na raha toka siku baba yako aliyoniomba tuzae nilianza kukupenda kabla sijapata mimba. Nilipo pata ndio uwii nilikua natamani siku ifike tuonane mwanangu sasa ndio nika zidi kumpenda baba yako vibaya sana Hahhahahah,” aliandika Faiza Instagram. “Nakumbuka siku moja na tumbo kubwaa baba yako akaniangalia nilikua na chupi tu hahaha nilikua niko bize nampangia nguo zake kabatini akaniambia sister du nime kukomesha nikamwambia aawapiiii huja nikomesha nafurahi Kila step ya mimba yangu. Sasha Mpenzi wangu stori ni nyingi sana siwezi kumaliza

USIRUHUSU SIMU YA MKONONI IWE SUMU KATIKA UHUSIANO WAKO

Image
Miaka ya nyuma, hususan wakati simu za mkononi zilipokuwa hazijaingia nchini, matatizo kwa wanandoa au wapendanao yalikuwa machache sana kulinganisha na sasa baada ya ujio wa simu. Ni wazi kwamba katika migogoro mingi ya mahusiano simu imekuwa kichocheo kikubwa cha wapendanao au wanandoa kugombana. Simu ndizo zinazoleta uhasama na kuvunja ndoa nyingi. Simu ndizo zinawafanya watu wengi waliopo kwenye uhusiano kugombana. Bahati mbaya sana, kati ya kesi nyingi za simu, zipo ambazo zinakuwa na ukweli lakini nyingine huwa hazina ukweli. Mtu anaanzisha ugomvi kwa sababu tu ujumbe wa kimahaba umeingia kwenye simu ya mke au mumewe. Hahitaji kuhoji. Anapoona tu ujumbe umeingia, kinachofuata ni ugomvi kwa mwenzi wake. Atamtukana, atampiga na atafanya kila linalowezekana kuhakikisha anaondoa hasira zake kwa kile alichokiona. Kumbe pengine angejipa nafasi ya kutafakari, akahoji, labda hata wasingefikia hatua ya kugombana. Anaanzisha ugomvi kumbe yule aliyetuma ujumbe huo

HIVI UNAITAMBUA THAMANI YA ULIYENAYE ?

Image
Najua wote tunajua thamani ya mapenzi na pia tunafahamu ni jinsi gani mapenzi yanatesa, yanaumiza na wakati mwingine kuua. Wengi tunafahamu jinsi mapenzi yalivyoleta umoja, undugu na urafiki ambao haukutarajiwa katika maisha yetu lakini kutokana na huyu kuoa yule na yule kuolewa na huyu tumejikuta tukiunganishwa na jambo hilo. Licha ya kujua thamani ya mapenzi na maumivu yake lakini tumeshindwa kuilinda thamani na kuyapuuza maamuvi yake. Tumekuwa wakosaji wakubwa sana kwa wenza wetu tulionao. Tumekuwa hatutambui thamani ya tulionao mpaka pale wanapoondoka mikononi mwetu. Tumekuwa watu tusiothamini mioyo na machozi ya wenza wetu kanakwamba sisi ni wanyama. Kwanini umlize mwanaume aliyekupenda na kukusaidia katika maisha yako? Kwanini umsaliti mwanamke aliyekupa mwili wake na moyo wake pamoja na kukupa thamani kubwa katika maisha yake? Ipi thamani ya machozi yake kwako? Ipi thamani ya mapenzi yake kwako? Kwanini uliache penzi lako lenye furaha na kwenda kwa mtu mwin

WANAWAKE WOTE WANAPENDA KUFANYIWA HAYA

Image
Nikikuuliza unapenda kipi kutoka kwa mpenzi wako najua wengi watatoa majibu tofauti tofauti wapo watakao sema, mcheshi, anamvuto napenda anavyo tabasamu na vitu vingine kama hivyo, LAKINI leo kupitia katika Mtembezi Mahaba karibu uyatambue mambo matatu muhimu ili kumdatisha mwenza wako. 1.UZUNGUMZAJI WAKO Unavyozungumza na mpenzi wako ni tofauti kabisa na unavyozungumza na watu wengine. Ni hatari sana kutumia lugha ya ukali ama isiyo ya kiungwana kwa mpenzi wako. Unatakiwa kufahamu kwamba, mpenzi wako ni mtu muhimu sana katika maisha yako hivyo unatakiwa kuwa makini pindi unapozungumza naye. Kuonesha kwamba wapo wasiojua mapenzi ni nini, unamkuta mtu anamuita mpenzi wake majina kama vile mshamba na mengine mengine kama hayo, Mpenzi wako kweli umuite demu? Na wale wengine kule mtaani utawaita nani? Huo si ustaarabu na kamwe mapenzi yenu hayawezi kushamiri kwa mtindo huo, Kuna wengine matusi haya waishi midomoni mwao. Kwa kufanya hivyo jua tu

NAMNA PEKEE YA KUEPUKA MAUMIVU KATIKA MAPENZI

Image
Siku zote mapenzi yanapofika ukomo huwa na visa kibao hali inayopelekea maumivu yasiyokwepeka, hivyo basi kwa kuliona hilo  Mtembezi Mahaba leo imekuandalia njia pekee za kukuepushia maumivu yasiyokuwa ya lazima katika mapenzi. JIFUNZE KUSAMEHE NA KUSAHAU: Hakuna jambo ambalo hutuliza fikra na hisia za mapenzi kama kukubali kumsamehe yule aliyekuudhi kabla hata hajakuomba msamaha na kuamua kusahau yote yaliyotokea. Yawezekana wengi mtasema haiwezekani. Marafiki, lazima kila mmoja aelewe kwamba unapokasirika au kuumizwa, anayeteseka siyo yule aliyekusababishia maumivu bali ni wewe mwenyewe. Hasira au maumivu ya kimapenzi huwa kama moto mkali ambao huitafuna taratibu nafsi ya mhusika.  Ukisamehe maana yake unaupa moyo na akili yako nafasi ya kupata sehemu ya kutulia na kuuzima moto ambao tayari ulishaanza kukolea ndani yako. BADILISHA MAZINGIRA/ MARAFIKI: Baada ya kuumizwa na mwandani wako, mbinu ya kubadilisha mazingira na marafiki husaidia sana