Posts

Showing posts from February, 2016

Tazama Video Mpya ya Harmonize Aliyomshrikisha Diamond Platnum....Imeanza Kuwa Gumzo Mtaani Hapakaliki

Image
Kutoka label ya Wasafi Classic ,Harmonize ameachia video mpya inayoitwa Bado aliyomshrikisha Diamond ambaye pia ni Boss wake

Sina Mpango wa Kuoa Mtu - Ney wa Mitego Afunguka..

Image
Msanii Ney wa Mitego amesema kwa sasa hana mpango wa kuoa na wala hafikirii kuoa, licha ya kuwa na watoto ambao wanahitaji malezi ya mama.Ney ameyasema hayo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kwa sasa hayuko kwenye mahusiano yoyote, na suala la kuoa kwake ni suala zito, hivyo hawezi kukurupuka na kuchukua uamuzi wa kuoa."Kusema kweli kabisa nimeulizwa swali ambalo sijaulizwa muda mrefu, na nikiulizwa huwa nalikwepaga, kufuatana na mahusiano ambayo nimekuwa nayo katikati, namshukuru Mwenyezi Mungu amenijalia watoto, for this time nikisema nizungumzie kuhusu ndoa nitadanganya, mi sifikirrii kabisa kuhusu kuoa for this time, kwa bahati mbaya au mzuri mi sipo kwenye mahusiano, sitaki kukurupuka, unajua ukifunga ndoa kwa sisi, mi ni mkristo hiyo ndo nitolee, yani hapo ndo umejicomit umeshaingia kwenye 18 ambazo huwezi kuzipangua tena, sifikirii kuoa, siwazi na sidhani kama nina huo mpango", alisema Ney wa Mitego.Pamoja na hayo Ney wa Mitego amekiri kuwa na mahusi

Polisi Yavamia Harusi, Wakamata Bwana Harusi na Watu Wake Kwa Kuhusishwa na Kesi ya Ujambazi Access Bank

Image
Baada ya kupitapita huku na kule katika maeneo yaliyotokea kadhia ya ujambazi jana nilifanikisha kunasa tukio Moja maeneo ya Chulwi Kongowe Mbagala kama sijakosea.Mnamo 27.2.2016 majira ya SAA 12 jioni polisi walivamia harusi iliyokuwa ikifungwa msikitini na kuwakamata watu waliokuwemo ndani wakiwatuhumu kuhusika na Ujambazi uliofanywa siku ya tarehe 26.2.2016 katika tawi moja la Bank ya Access lililoko Mbagala.Raia walisema polisi ilivamia msikiti na kuwakamata walimu wa dini waliokuwa wakifungisha ndoa hiyo na kuwachukua na kwenda nao hadi ilipo harusi na kuwakamata wengine huku wakiwapiga na kuwatuhumu kuwa wamehusika na ujambazi.Hata hivyo polisi ilimwachia huru bibi harusi na kuondoka na babu harusi na wapambe wake sehemu kusiko julikana.Miongoni mwa watu waliokamatwa ni Abdullah Saudi, Juma selemani, Saidi Ally na kassimu Othuman wote wakiwa wakazi wa Mbagala waliokuja kusheherekea harusi ya rafiki yao.

Unajua Athari za Kuitana Sweet, Dear na Baby Kwa Watu Ambao Sio Wachumba ama Mke na Mume?

Image
BABY ni neno la Kiingereza lenye maana ya mtoto, tena mara nyingi linatumika kwa mtoto mdogo. Pia lina maana nyingine ya mpenzi. Ni neno maarufu sana siku hizi; hata wazee kabisa, utasikia wanaitana baby! Mbali na hilo, yapo maneno mengine kama sweet, dear, honey na mengine mengi. Maneno yote hayo ya Kiingereza, yana maana zaidi ya moja, lakini kubwa zaidi ni kumaanisha mpenzi, mpendwa (hutumika katika kuonesha mapenzi ya dhati kwa mwingine). Leo nataka kukupa kitu kipya kabisa kichwani mwako. Unahitaji utulivu wa hali ya juu ili kujifunza hili. Ni maneno mazuri sana, ya kipekee lakini kwa upande mwingine ni hatari kwa sababu hukaribisha matatizo ambayo hayakutarajiwa na mtumiaji. HUTUMIKA WAPI HASA? “Dear, naomba uniamshe saa 12:00 asubuhi, kesho nina vikao vingi sana asubuhi,” inaweza kuwa kauli ya mume akimwambia mkewe, ambaye naye anamjibu: “Sawa sweet, usijali.” Kwa hakika ndipo sehemu sahihi zaidi kutumika. Ni maneno yenye mshawasha mkub

Mambo 20 Ya Kufanya Kudumisha Uhusiano Wako Siku Zote.

Image
1. FANYA UCHAGUZI SAHIHI Hapa ndipo watu wanapotakiwa kutumia akili zao mpaka zile za akiba, ukikosea hapa ni rahisi sana kuvurunda hapo baadaye. Uhusiano wenye nguvu, hujengwa na penzi la kweli. Acha kukurupuka, lazima ujihakikishie kwamba uliyenaye ni chaguo kutoka ndani ya moyo wako. Najua una maswali; kwamba utawezaje kumjua mwenye mapenzi ya kweli, hiyo ni mada ambayo nimeshaandika mara kadhaa katika ukurasa huu na gazeti damu na hili, Ijumaa. Kimsingi, kwa kufuata maelekezo hayo, mwenzi ambaye unatarajia kuwa naye katika maisha ya ndoa hapo baadaye, lazima msingi uwe ni uchaguzi sahihi. Sikia, watu wengi waliokuwa na fedha, wamefilisika baada ya kuoa/kuoleawa na wenzi ambao si sahihi. Aidha, wapo wenye mafanikio makubwa sana, ambayo wameyapata baada ya kuoa/kuolewa na wenzi sahihi. Rafiki zangu, si jambo rahisi kumpata yule aliye sahihi. Inahitaji utulivu. Yapo mengi sana ambayo unapaswa kuyaangalia, ambayo nimekwishaeleza sana katika mak

Picha Raisi Obama Akiwa na Watoto Ambazo Zimegusa Hisia za Wengi, Zipo Hapa

Image
Rais wa Marekani, Barack Obama ni miongoni mwa watu wanao pendwa, huu ni uthibitisho ambao wengi wanaweza kukubaliana nao. Katika mafanikio yake katika siasa na ukaribu na watu umemfanya watu wengi wawe wanampenda lakini kupitia picha hizi akiwa na watoto zimegusa hisia zaidi. Obama hajawahi kuwa mtu wa kuzuia hisia zake, Kama akifikwa na machozi basi hata mbele za watu hutokwa na machozi, Picha hizi zilizo wekwa mandaoni zikiwa na hashtag #ObamaAndKids zimeonyesha hisia zake kwa watoto.

JE Wanawake Mnafahamu Nguvu Za Pekee Mlizopewa Na Mungu ?

Image
Wanawake wangejua thamani ya Nguvu waliyopewa na Mungu wasingekuwa viumbe wanyonge kama walivyo sasa..Wale wachache wanaojua nguvu iliyo ndani yao,muda wote watakuwa wanaonekana TOFAUTI/HADIMU..Wanawake wamepewa nguvu ya kubalisha kitu chochote hata vile vigumu vilivyoshindikana.  Shida yenu mko bize kubetua nyonyo, kupiga selfie na kubenua makalio..Mtalia sana.. Adam na akili zake zote na kupendwa kote na Mungu na kupewa bustani ya Edeni lakini Eva alimshawishi na tunda akala akatucost mpaka leo tunakufa... Samson alikuwa mtu mwenye nguvu sana,na siri ilikuwa nywele,wote hawakujua siri lakini Delila alimtongoza mpaka Samson akatoa siri,Wafilisti wakamtenda..  Mfalme Daudi alipendwa na Mungu,akawa mfalme,akamuua Goliath lakini ujanja wote akaishia kupiga chabo mke wa mtu, akazini nae,akamuua na mmewe ili afaidi mke wa mtu..Ikamcost... Power of a Woman...Kama wewe ni Mwanamke na unachojua ni kulalamika na kulialia tatizo sio la Mungu ni la kwak

Rekodi Hii ya Mwanamuziki Michael Jackson Yavunjwa na Rihanna.

Image
  Single mpya ya muimbaji huyo mwenye miaka 28, Work aliyomshirikisha Drake, imekuwa ya 14 kukamata nafasi ya kwanza kwenye chati za Billboard Hot 100 na kumshinda Michael aliyekuwa na nyimbo 13. Rihanna bado yupo nyuma ya Mariah Carey, mwenye nyimbo 18 huku The Beatles wakishika rekodi ya dunia kwa kuwa na nyimbo 21.

Aika asema Nahreel huwa ana mpangia cha kuvaa japo yeye hampangii

Image
Mwanadada anayeunda kundi la Navy Kenzo amefunguka na kusema kuwa mpenzi wake Nahreel ambaye pia ni member wa kundi hilo huwa anamsaidia inapofika swala la kuchagua nguo za kuvaa. “ huwa ananisaidia kwa kweli,huwa ananipa advice kwamba hiyo haijakupendeza na vitu kama hivyo ” alifunguka Aika. Kwa upande wake Aika alipoulizwa kama huwa ana mpangia Nahreel cha kuvaa alisema,” Nahreel kila mara anakuwa na staili tofauti ni mtu ambaye anapenda kuji discover kwa hiyo inakuwa ngumu kumpangia kila anachovaa unaona amependeza ”

Baraka da Prince kutoa ngoma na Ali Kiba,aeleza anavyomzimia.

Image
Msanii wa bongo fleva Baraka da Prince ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake wa siwezi ameweka wazi kuwa pengine baada ya wimbo wake huo wa sasa huenda akatoa ngoma ambayo amefanya na Ali Kiba. Baraka pia amefunguka na kusema kuwa yeye ni mshabiki mkubwa wa kazi za Ali Kiba ukiachana na ukweli kwamba yeye na Kiba ni kama mtu na mdogo wake kimuziki. Kupitia mahojiano na redio moja Baraka alisema “ mimi ni mshabiki mkubwa sana wa Kiba,napenda kazi zake..nilihasa kama nahitaji kufanya nyimbo na mtu na nikamfikiria jamaa mwenyewe awe Kiba,nilipoongea akaitikia poa akaniambia kuna utaratibu niufuate kwa kuwa yeye yupo chini ya menejimenti,nikafata utaratibu tukaingia studio tukawa tumepiga kitu ” alifunga Baraka na kuongeza ngoma hiyo itatoka hivi punde.

Picha, Saa ya Davido yenye thamani ya shilingi milioni 264 za Tz

Image

Tetesi,Bow wow anatoka na Keyshia Cole na wanategemea kupata mtoto.

Image
  Rapa/Mtangazaji Bow Wow ameripotiwa kuwa na mahusiano na msanii wa rnb Keyshia Cole na kwamba wanategemea kupata mtoto. Tetesi zinasema Bow Wow ameondoka kwenye nyumba ya Erica Mena na kuhamia kwa Keyshia Cole. Kwa mujibu wa rafiki wa Keyshia Cole “Bow wow amekuwa karibu na Keyshia kwa muda sasa,hawako serious sana ila Keyshia anamimba na amesema anazaa”

Picha za Bien-Aime Baraza wa Sauti Sol na mpenzi wake Mnigeria

Image
Mwimbaji wa Sauti Sol Bien-Aime Baraza ambaye amemuweka wazi mpenzi wake hivi karibuni amesema sababu za kuweka mapenzi yake siri ni tatizo lake Binafsi na sio kwamba hapendi watu wajue maisha yake ya kimapenzi. Bein anajulikana kwa kulikimbia swali na Nani ni mpenzi wako kwenye kila interview ila mwaka huu kamwaga yote. Mpenzi wake ni ‘Chiki Onwukw’ ambaye ni Mnigeria anayefanya kazi kama dancer na mwalimu wa Fitness.

Picha,Avril na kovu usoni.

Image
Baada ya tetesi kuwa amebwagwa na mpenzi wake kwenye siku ya wapendanao mwezi huu, mwimbaji Avril ameonyesha kuendelea na maisha yake kama hakijatokea kitu vile. Avril aliweka picha akiwa na kovu usoni iliyoshtua mashabiki wake, wengi wakidhani ni kibigo alichopewa na mpenzi wake ambaye wametengana kwa sasa ila baadae iligundulika kuwa ilikuwa ni sehemu ya muonekano wake kwenye filamu mpya anayofanya sasa. Filamu inaitwa Sumu La Penzi na Avril anaigiza.

Babu Tale kumfanya dogo Janja aimbe,mwenyewe amesapoti hilo.

Image
Meneja wa Tip Top connection ambaye pia ana mmeneji Dogo Janja amesema muda wowote kuanzia sasa msanii huyo atasikika akiwa anaimba tofauti na staili yake ya kurap ambayo wengi wameizoea. Meneja huyo amesema kuwa yeye ni mfanyabiashara na anatoa vitu ambavyo vinahitajika sokoni ambapo anaamini kwa sasa muziki wa kuimba na kuchezeka ndio uko sokoni huku akitolea mfano wasanii wa Hip Hop waliobadilika wakiwemo wakina Madee,Professor Jay na kimbunga. “ madee alikuwa ana rap,lakini alipotoka na pombe yangu ikawa ndo nyimbo iliyomuingizia myimbo kuliko zote,ikamfanya ahamie nyumbani kwake..anytime Janja anaimba,humu kagusia goma lingine anaimba yote ” alifunguka Babu Tale wakati anatambulisha wimbo mpya wa Dogo Janja kwenye redio moja. Kwa upande wake Dogo Janja alionekana akisapoti hilo kwa kusema,” siku hizi hatuokoi Hip Hop,tunaokoa maisha ” Source: Clouds

KIFO: February 25 2016 Tanzania imempoteza mkongwe mwingine wa muziki

Image
Ni Kassim Mapili … mwimbaji mkongwe lakini hata kijana wa sasa hivi atakua amesikia sana moja ya nyimbo zake kubwa za wakati wote…. ina maneno….. ‘ napenda nipate lau nafasi…. nipate kusema nawe kidogo rohoni naumiaaaaaa ‘ Rais wa shirikisho la Wanamuziki Tanzania Addo November amesema ‘ Mzee Mapili hivi karibuni alikua anasumbuliwa na matatizo ya moyo akawa anatibiwa na akapona kabisa na kuendelea na majukumu yake ya kawaida lakini jana aliporudi nyumbani hakutoka tena ‘ ‘ Mzee alikua na vijana watatu lakini hakuwa anakaa nao pamoja na hata mke wake walishaachana, jana alipoingia chumbani kwake hakutoka… majirani walikua wanajua ana tabia ya akiingia kulala anaweza kutoka kesho yake mchana ila leo hakutoka, ikabidi waende Polisi wakaja kuvunja mlango na kukuta alishafariki ‘ – Addo November.

Masikini Ray C Afunguka Tena..'Nilianguka Bahati Mbaya Kama Binadamu Mwingine Watu Wangu wa Karibu Wamenitenga'

Image
Ray C ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha Planet bongo kinachorushwa na kituo cha EATV . ''Nilianguka bahati mbaya kama binadamu wengine ,nikajitambua sasa nipo vizuri naendelea na maisha kama kawaida japo nakumbwa na changamoto ya kutopata usaidizi kutoka kwa watu wangu wa karibu niliokuwa nao kwenye musiki zamani''Amesema Ray C Msanii huyo amemshukuru Rais Mstaafu Jakaya Kikwete kwa kumchukulia kama mwanae na kumsaidia kupata matibabu baada ya kutumia madawa ya kulevya na kumuathiri kwa muda mrefu. Aidha ameiomba jamii kumpokea na kumuunga mkono katika kazi zake ambazo anazifanya ambapo kwa sasa amerekodi nyimbo 5 na kuwataka waandaaji wa vipindi vya redio,televisheni na magazeti badala ya kila siku kumuandika vibaya wamuunge mkono katika jitihada zake za kurejea kwenye hali ya kawaida. ''Kuna magazeti kazi yao ni kuniandika vibaya kila siku mara nimeonekana n

Naibu Spika Dr Tulia Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali Mbaya ya Gari....Nimekuwekea Picha za Ajali Hapa

Image
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kupata ajali jana jioni. Taarifa za awali zimeeleza kuwa Dk. Tulia alipata ajali hiyo baada ya gari dogo kugonga gari alilokuwa akisafiria katika eneo la Kiwira jijini Mbeya. Blog Lists DAR ES SALAAM WIRE KIA told to boost collections - THE government has ordered the Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO) which operates the Kilimanjaro International Airport to increase revenue ... Nafasi za Kazi Tanzania Nafasi ya Kazi Ifakara Health Institute (IHI), Application Deadline 29 February 2016 - *IFAKARA HEALTH INSTITUTE (IHI)* *ADVERT* TITLE: Data Use Coordinator. REPORTING: To Chief Research Office IHI LOCATION: Dar es

Kundi la Navy Kenzo Kufanya Show Kubwa Kwa Mara ya Kwanza Maisha Basement Jumapili Hii 28 Feb 2016..Usikose Kamatia Chini

Image
Kwa Mara ya Kwanza Kundi la Navy Kenzo litafungua Kamatia Tour Maisha Basement Club Dar Jumapili hii Tarehe 28 Feb...Njoo Uone Nahreel Anavyomkamatia Baby wake Aika..Pia mtawaona wakiimba Game, Viza, Bokodo na Nyimbo zao nyingine Kali ... Usikose Kiingilio ni 10,000 mlangoni Blog Lists DAR ES SALAAM WIRE KIA told to boost collections - THE government has ordered the Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO) which operates the Kilimanjaro International Airport to increase revenue ... Nafasi za Kazi Tanzania Nafasi ya Kazi Ifakara Health Institute (IHI), Application Deadline 29 February 2016 - *IFAKARA HEALTH INSTITUTE (IHI)* *ADVERT* TITLE: Data Use Coordinator. REPORTING: To Chief Research Office IHI LOCATION: Dar es Salaam Summary Ifakara H...