Kuliko Nitoke Kimapenzi na Msanii, ni Bora Hata Nitoke na Msukuma Mkokoteni – Ray C



Msanii wa muziki Ray C amedai hawezi toka kimapenzi tena na msanii kutokana na kuumizwa na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Lord Eyes.

Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha ENewz cha East Africa Television kuwa toka aachane na Lord Eyes hajawahi kuingia tena kwenye mahusiano na kudai kuwa msanii huyo alimuumiza sana mpaka yeye kuingia kwenye matumizi ya dawa za kulevya kipindi hicho.

“Kwa sasa bado sina boy friend, now nina marafiki tu kiukweli nafasi hiyo bado maana Lord Eyes aliniumiza sana, nilimpenda sana na ndiyo maana nilifanya alichokuwa akifanya, sikutegemea kama ingekuwa vile, hata kwenye drugs unakutana na rafiki yako anafanya hiki na wewe utataka kufanya ili aone upo naye pamoja, ila kwa sasa mimi na wasanii hapana, ni bora hata nitoke na msukuma mkokoteni ili mradi anipende maana mimi nina mapenzi ya kweli ndiyo maana unaona hata nyimbo zangu nyingi ni za mapenzi” Alisema Ray C.

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016