Matikibokoyao: Wema Sepetu Rudisha Pesa za Nguo Unazodaiwa na Manyota



Aliyekuwa shabiki namba moja wa muigizaji wema sepetu(Team wema) , matilda au maarufu kama matikibokoyao ametoboa moja ya siri ya aliyekua boss wake kuwa huwa anakopa nguo kwa mfanyabiashara maarufu mjini aitwaye manyota, hivyo amemtaka msanii huyo mpenda kick mjini aende akalipe madeni ya watu.

Akiendelea kumwaga ubuyu, Yuda huyo hakumuacha nyuma muigizaji lulu michael na kudai kuwa na yeye pia ana madeni sugu kama ilivyo kwa boss wake(Wema).

Chanzo cha bifu hicho inasemekana ni mimba aliyokua nayo staa huyo(wema) ambapo inadaiwa mfuasi wake huyo nambari moja amekua akitembeza ubuyu kwa maadui zake(wema) kuhusu ujauzito wake ambapo boss huyo aliamua kumchana live kijakazi wake huyo na kumkana hadharani kuwa hamjui.

Bifu hilo liliendelea mbele zaidi ambapo shabiki huyo wa madame aliapa kutoboa siri kibao za boss wake huyo , hata hivyo baadae madame baada ya kuona mambo yake yanaanza kuanikwa alianza kujirudi taratibu kwa mfuasi wake huyo na kuyamaliza kiutu uzima

Chanzo: Jamii Forums

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016