Posts

Showing posts from April, 2016

Video ya Chura Yawa Gumzo Mtandaoni..Hivi Ndivyo Inavyozungumziwa nje na Ndani ya Tanzania

Image
Video ya Mwanamuziki Snura iliyotoka hivi Karibuni imekuwa gumzo mtandani kwa jinsi wadada wanavyotingisha makalio kwa mtindi wa Chura kama jina la wimbo huo unavyoitwa..Japo video hiyo mpaka sasa haijachezwa na kituo chochote cha Tv Tanzania lakini huko Youtube inaonekana imeshakuwa maarufu kwani watu nje ya nchi na ndani wamekuwa wakiijadili kwa maoni tofauti tofauti Hapa nimekuwekea maoni mbali mbali ya Wadau: Boss Hogg2  Thats it am going to TZ... Hey tanzanians, place gani poa ya kupata madem wana mizigo huko kwenu... Area gani na club gani.. Mtu anijibu Ado Ashu1 Astaghfirullah!! Mna laana wote mliojidhalilisha ktk hii nyimbo. Ama kweli thamani ya mwanamke inapotezwa na watu wachache kama nyie. Niyongabo Idrissa Mnaosema video haina maadili mnatafuta nini youtube? La Shay Glenn2  Wanaosema hii tradition mjiulize kwa nini snura asijiweke hapo,halaf hao wanawake wamevaa mask....obvious its wrong in many ways emanuel kilima10  Oooops ladies and gentle

Hatimaye Lulu Michael Avishwa Pete ya Uchumba na Dj Majay...Tazama Picha Hapa

Image
 Lulu Amepost Picha Kadhaa Akionyesha Pete yale aliyovalishwa na kuandika maneno haya: Simplicity z the key. Kwenye picha nyingine ameandika: Pale unaposikia Kwa…Kwa…Kwa…Kwa Ya Rihanna wakati WA kupiga picha #simplicityisthe

Madawa ya Kulevya yamponza Mwanamuziki Ferooz...Mwenyewe Asema Haya

Image
Baada ya ukimya wa muda mrefu sana wa wakongwe wa muziki wa Bongo Flava story zilizopo mtaani ni kuwa Ferooz ni miongoni mwa wasanii wanaotumia madawa ya kulevya na ndiyo sababu iliyompoteza kwenye reli ya muziki. Kupitia Enewz Ferooz alikanusha tuhuma hizo na kudai kuwa misongo ya mawazo ndo huwa inawapelekea wasanii kuingia katika matumizi hayo ya madawa ya kulevya na kuwataka wengine wasifanye hivyo. Ferooz amesema kuwa “Ni mara kumi upate UKIMWI kuliko uwe unatumia madawa ya kulevya” lakini pia akaongezea kwakusema “Nawashauri watu wengine pamoja na wasanii wenzangu wasije wakajaribu kufanya hivyo”.

Jambazi Sugu la Tigo Pesa Lakamatwa Dar es Salaam , Wenzake Wawili Watoroka

Image
MTU MMOJA ANAYE SAKIKIKA KUWA JAMBAZI AMEKAMATWA JIJINI DAR MAENEO YA POSTA BAADA YA KUTAKA KUMTAPELI MAMA MMOJA ANAYE FANYA KAZI YA TIGO PESA … MASHAHIDI WALIO KUWEPO ENEO HILO WANASEMA HUYO KIJANA ALIFIKA KWA DADA HUYO KWA LENGO LA KUTAKA KUWEPA PESA KIASI CHA TSH.ELFU TANO .. WAKATI YULE DADA ALIKUWA ANAHESABU PESA ZAKE KWANZA NDIPO HUYO JAMBAZI AKAKWAPUA NA KUKIMBILIA NDANI YA GARI AINA YA NOAH..NA KUMRUSHIA MTU ALIYEKUWA NYUMA YA HILO GARI…. WAKATI HUO MCHEZO UKIENDELEA NDIPO DEREVA AKAWA ANAJIANDAA KUWASHA GARI NA KUONDOKA NDIPO RAIA WAKAMDAKA DEREVA NA KUMTOA KWENYE GARI  …LAKINI DEREVA NA YULE ALIYEPOKEA PESA AKACHOROPOKA ..ILA YULE ALIYEIBA AKANASWA NDO HUYO KWENYE PICHA

Nay Aliachwa na Shamsa Ford Sababu ya Vibomu-Niva

Image
Msanii wa filamu nchini Niva Super Mariyoo, ambaye alionja joto ya jiwe kwa muda fulani baada ya kutajwa kwenye wimbo wa Nay wa Mitego 'Shika adabu yako' na kusema "Huyo msanii huyo hana hata chumba cha kupanga ila anaishi kwenye gari". Niva amefunguka na kusema kuwa Nay wa Mitego siku zote huwa anaimba watu maarufu ili apate kiki na kusema msanii huyo kutokana na kufanya nyimbo mbovu mbovu ndiyo maana hata siku moja hajawahi kupata tuzo. Akizungumza kwenye kipindi cha eNEWS Niva Super Marioo amedai kuwa ni kweli kwa sasa wanawake wengi wanafanya kazi na kutafuta riziki na wanakuwa wanawasaidia baadhi ya wanaume ambao kazi yao kukaa nyumbani kama Imma Chogo ambaye ni (Nay wa Mitego). "Kimaisha mimi Imma Chogo hajanifikia sema sisi wengine huwa hatupendi kujiweka wazi sana, kama kweli mtu unamiliki nyumba, una kwako kwanini hutulii na familia? kama kweli wewe unajiona ni Gentle Man kwanini wanawake wanakukimbia? Star anakimbiwa? mimi najua Star

HASARA YA MAPENZI YA KUCHUNGUZANA

Image
  Katika maisha mawazo ni kitu cha kawaida kwa mwanadamu, lakini hata hivyo matumizi ya akili lazima yawekewe mipaka na isiwe ni kitu cha kawaida Ubongo kuruhusiwa kwenda mwendo mkali kulingana na uwezo wake. Hebu chukua jukumu la kuutazama ulimwengu huu tulio nao na uangalie uozo wa wanadamu katika kujiheshimu, kisha ujiulize hivi kuna mwanaume au mwanamke ambaye anaishi bila kumsaliti mpenzi wake?  Baada ya swali hilo wachukue rafiki zako unaokunywa nao pombe na kufanya kazi nao kazi uone kama hamjawahi kuoneshana nyumba ndogo, baadaye fumba macho uiulize akili yako kuna asiyesalitiwa?. Wakati unasubiri majibu endelea kuweka viashiria kichwani mwako kwa kumfikiria mkeo anayemhudumia bosi chai huko ofisini au Muuguzi anayefanya inashangaza kusikia na kuona kuna baadhi ya wanandoa wanaishi kwa kupelelezana kila siku kama askari wakaguzi wa dawa za kulevya. Mke akichelewa kurudi lazima akaguliwe kwanza kama hakutoka kupasha mwili nje, kadhalika mwanaume  apimwe kwa

Mrembo Jack Wolper Afunguka Sababu za Kuacha Kuvaa Nguo za Kiume

Image
Akiongea kwenye kipindi cha Nirvana, kinachoruka kupitia EATV, Wolper alisema ‘nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule, sasa hivi nimeshakuwa na mchumba’. “Nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule ulivyokuwa. Kuna watu walikuwa wanapenda, lakini sasa hivi nimeshakuwa mchumba wa mtu. Ni kweli lazima nivae gauni, kwahiyo mtu unatakiwa ujibadilishe wewe mwenyewe usisubiri kubadilishwa,” aliongezea. Wolper aliendelea kusema, “hata hivyo bado sijaacha kabisa, kidogo unakuwa unagusia mashabiki zako wanakuwa wanakupenda.” Hata hivyo Wolper japo amekiri kuwa na mchumba mpya kwa sasa lakini hayupo tayari kuweka mahusiano yake hadharani kama mwanzo alivyokuwa anafanya.....

Namuona Mwanamuziki Harmonize Ndani ya Diamond Platnumz

Image
Moyowe ya Afande Sele akiwa na Jay mo moja kati ya nyimbo zangu chache ambazo huzisikiliza mara nyingi kwa siku. Moja ya kati ya maneno yenye busara aliyosema Afande Sele ni “Hii ni fani na msanii na msanii siko mwenyewe ili nifanikiwe inahitaji nikosolewe na inapobidi nisifiwe” Kwa wafuatiliaji wa muziki hakika Harmonize si jina jipya katika masikio yao, Aiyola ni wimbo wake uliomtambulisha kwenye ramani ya bongo fleva yani muziki wa kizazi kipya mwaka 2015. Aiyola ni wimbo ulifanyika katika studio za WCB ambazo zipo chini ya msanii Diamond Platnumz ambapo Rich Mavoko na Ray Vanny ni miongoni mwa wasanii waliopo chini ya Label hiyo ya WCB. Inadhihirika katika maisha ya binadamu kabla ya kutokea chochote basi lazima kuwe na ishara yoyote ile, kabla ya kutoka kwa Harmonize hakika ishara zilikuwepo hasa kwa wale wanatumiaji mtandao wa picha Instagram. Tulipata kuona tambo za msanii Diamond pamoja na wapambe wake wakiwa wanampamba na kumnadi msanii huyu chipukizi Harmon

Mauaji Nyumba ya Kulala Wageni..Mfanya Biashara Akutwa Kachomwa Kisu Shingoni

Image
Mfanyabiashara wa mazao, Eliusta Peter(40),   amefariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni akiwa katika  nyumba ya kulala wageni wilayani Kilombero. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alisema tukio hilo lilitokea   Aprili 22  baada ya  wahudumu wa nyumba  ya wageni ya  Sayari kubaini   maiti katika chumba namba mbili. Inadawa Aprili 20 mwanamke huyo  akiwa na kijana mmoja ambaye  jina lake limehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi, walifika kwenye nyumba hiyo na kuchukua chumba kimoja wakisema  wao ni wafanyabiashara wa mazao. “Mwili wa marehemu uligundulika ukiwa kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Sayari chumba namba mbili   saa 11 jioni na ulipochunguzwa ikagundulika kuwa kifo kilisababishwa maumivu ya jereha,”alisema Matei. Mwanamke huyo  alikuwa na jeraha   kushoto mwa bega lake lililotokana na kuchomwa na kitu chenye ncha kali Matei  alisema kwa taarifa walizozipata  bila shaka kijana aliyekuwa naye  anahusika na mauaji hayo

Hizi ni Dalili za Mwanamke Anayekupenda Kwa Dhati Toka Moyoni, ila Hawezi Kukuambia

Image
Kumekuwa na imani potofu kwa wanawake kwamba hawawezi kumwambia ukweli mwanaume anampenda kwanza mpaka mwanaume aanze lakini ukweli usiopingika ni kwamba wao pia hupendi na mara nyingi wao wakianza kupenda hupenda kweli kufikia stage hata ya kuhisi kuumwa. Hizi ni dalili za mwanamke anaekupenda ila anagoma kukwambia tu. 1. KUKUTEGA ILIKUJUA THAMANI YAKE KWAKO Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda na kumthamini au la mfano wa mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake. 2. KUPENDA KUCHEKA TENA MUDA MWINGINE KWA NGUVU Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli. 3. WIVU Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unachart nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi na hupenda yale afanyiwe yeye tu hata kama sio mpenzi wako. 4.HUKUMBUKA MATUKIO MUHIMU YOTE

Faiza Ally Awajibu Mashabiki Wanaomtag Kuhusu Sugu Kumnunulia Gari Mpenzi wake Mpya..

Image
Instagram siku hizi kimekuwa ni kiota cha umbea wa mjini, Alhamisi hii akaunti moja maarufu ya umbea imeweka picha ya mwanadada anayedaiwa kuwa ni mpenzi mpya wa mbunge wa Mbeya, Mh Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ pamoja na gari ambalo anadaiwa kuzawadiwa siku yake ya kuzaliwa. Akaunti hiyo ilipost picha (hapa juu) na kuandika: Sugu shikamooo!ahsante kwa kutunyoosha sio kwa bday zetu zile za kiingilio na za kusaka wafadhiri miezi 3!kha hilo lizawadi toka kwa baby ni funga kazi..mtatoo umetulia hata ukiachwa huna haja ya kufuta bana raha si ulishazila bana?? jamani wagonjwa wanaendeleaje huko ICU??…Ukishindana na moto lazima ukuunguze dadeki Post hiyo ina komenti tofauti tofauti ambapo baadhi ya mashabiki waliamua kumtag mpenzi wa zamani wa Sugu, Faiza Ally ambaye alizaa naye mtoto mmoja aitwae, ‘Sasha’. Faiza Ally ambaye kwa sasa yupo nje ya nchi aliamua kujibu na kuandika: Mmnanitag ili iweje ? watu wamenunuliwa magorofa kariokoo itakua harrier  people g

Mwili wa Papa Wemba Wawasili Kinshasa Congo...

Image
Mamia ya watu wamekongamana nje ya uwanja wa ndege wa Kinshasa kuupokea mwili wa mwanamuziki Papa Wemba uliowasili nchini humo kutoka Abidjan Mwanamuziki huyo ambaye ametajwa kuwa mmoja ya waanzilishi wa muziki wa kizazi kipya cha Soukous anatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne baada ya mwili huo kuwekwa katika uwanja wa mpira kwa raia kutoa heshima zao za mwisho. Maafisa wa serikali na wanadiplomasia watahudhuria ibada ya kumkumbuka mwanamuziki huyo katika uwanja wa ndege kabla ya mwili huo kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti. Tamasha la bure la usiku kucha lilifanyika mjini Abidjan ambapo mwanamuziki huyo alianguka alipokuwa akiimba.Mwanahabari wa BBC Tamasin Ford anasema kuwa mashabiki wengi walivalia nguo nyeusi na kubeba mishumaa ili kutoa heshima kwa nguli huyo wa muziki. Mkewe Papa Wemba na wasaidizi wake pia walikuwepo.

Madai ya Kalio Feki la Wema… Mama’ke Afunguka

Image
Madai ya staa mkubwa Bongo aliye pia Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu kwamba wowowo lake linazidi kuwa kubwa kwa sababu anatumia dawa za Kichina yanazidi kushika kasi huku kwa mara ya kwanza mama yake mzazi, Mariam Sepetu akifunguka, Amani limechimba ukweli. MADAI YALIPOANZA Mashoga wanena, alianza na kuongeza unene, sasa kahamia kwenye makalio ili awe na wowowo. Manenomaneno hayo yakazidi kushika kasi zaidi kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kitu ambacho kinadaiwa kuikosesha amani familia ya staa huyo na hata yeye mwenyewe. Kulikoni jijini Mwanza, Pati ya Instagram yazua mjadala. Wa mtandaoni wao wanasema Wema anatumia dawa za Kichina kukuza ‘tela’ lake. WEMA ALIPOTAFUTWA Agoma kupokea simu. Agoma kujibu ujumbe. mamawema1Mama Wema MAMA YAKE MZAZI SASA “Nawashangaa wanaomsema vibaya mwanangu kuwa amejaladia (wowowo), wengine wanasema anatumia dawa za Kichani, hakuna ukweli wowote kwani Wema ni mwanangu, namjua alivyo. Hakuna kitu alicho-ongeza kwenye mwil

Ni kweli Diamond na Zari Wanataka Kuachana? Ni kweli Diamond Kahamishia Majeshi kwa Mrembo Lyn?

Image
Kinachoendelea sahizi instagram ni Mtifuano na ukorochoaji wa Maisha ya watu! Watu wapo busy,watu wapo katika pirika pirika za kutafuta ukweli kujua nini kinacho endelea kati ya Zari na Diamond na Diamond na Video queen wa Kwetu' Mama Diamond na mkwe wake na mawifi mtu! Kama unavojua wabongo Umbea una nguvu kuliko Ripoti ya CAG insta kumechafuka.....Mama Diamond alianza kwa kufuta picha zote alizo post za Zari watu wakasema Mmmmmmmmh kuna kitu hapa,(mimi sidhani kama kufuta picha za mtu ni kitu kibaya lakini hakufuta za zari tuu mbona hata za wengine alifuta akaacha za Tiffa na Rommy tuu) Wafuatiliaji wa mambo hawakuishia hapo wakasema Esma dada wa Diamond Ka muunfollow Zari (sina uhakika lakini Kwa usawahili wa huyu Dada nilishangaa kuona anapatana na Zari huyu ni mswahili mno na Diamond asipo kuwa Makini atamponza kwa uswahili wake) Watu wakaendelea na story kwanini Zari hakutoa shout out kwa wimbo wa Raymond video ya Kwetu wakaguna wakasemaaa mmmmmmmmh hapa ku

TID Afunguka 'Nilikuwa Natoka na Wema Sepetu Alafu Akaniambia Hanitaki..Sasa Hivi Akitaka Kurudi Hakuna Nafasi Tena'

Image
Akiwa Katika Kipindi cha Clouds 360 leo Mwanamuziki TID Amefunguka Kuhusu Kutoka na Wema Sepetu... "Nilikuwa "namdate" Wema Sepetu akaniambia Sikutaakiiii....tangu kipindi hicho nimekuwa na Wasichana wengi...Ikitokea Wema Sepetu anataka kurudi hakuna nafasi Tena"I'm occupied". Pia TID Amemuongelea Mwanamuziki Ommy Dimpoz na kusema kuwa yeye ndio aliyemtoa  "Alikuja studio kwangu akiwa anavaa ndala na kupitia kwangu alijuana na watu muhimu kama Ali Kiba na Ruge Mutahaba". Anasema pia yeye anapenda na ni bora afanye video zake hapahapa Tanzania ili kuitangaza nchi yetu na vivutio vyake zaidi.

Mh Mbunge Sugu Amnunulia Mpenzi Wake Gari Mpya Aina ya Lexus..Yazua Gumzo Mtandaoni

Image
Ripoti kutoka mitandaoni zinasema kuwa Muheshimiwa Mbunge Sugu Amemzawadia Gari aiana ya Toyota Lexus kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwa mpenzi wake ajulikanae kama Happiness, Sugu na mpenzi wake huyo mpya wamekuwa gumzo mitandaoni hasa baada ya aliyekuwa mpenzi wa Sugu wa zamani Faiza Ally kusema bado anampenda Sugu....Wadau wengi tunasubiri kuona Faiza atasema nini kuhusu hilo kwani amekuwa sio mvumilivu wa kukaa kimya kinapokuja suala la Sugu Hizi Hapa ni Baadhi ya Comments kutoka kwa wadau mitandaoni: mrs_j6316 @mwakobadoris  :njoo umuone Mrs sugu au first lady was Mbeya yetu mpaka raha wallah afu ametulia hadi uso full_mikuki  :Maskini bahati hizi wengine acha tuzae tu fine_mushy: Tenaaaaaa sio Harrier bubu Maana Kuna Harrier Kma Harrier mamaeeeee kitu LEXUS hiooooo official_chagga_girl: Kuna watu wanakufaa ukoo,haaa haaa @tit4tati

Mrembo Jack Wolper Afunguka Sababu za Kuacha Kuvaa Nguo za Kiume

Image
Akiongea kwenye kipindi cha Nirvana, kinachoruka kupitia EATV, Wolper alisema ‘nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule, sasa hivi nimeshakuwa na mchumba’. “Nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule ulivyokuwa. Kuna watu walikuwa wanapenda, lakini sasa hivi nimeshakuwa mchumba wa mtu. Ni kweli lazima nivae gauni, kwahiyo mtu unatakiwa ujibadilishe wewe mwenyewe usisubiri kubadilishwa,” aliongezea. Wolper aliendelea kusema, “hata hivyo bado sijaacha kabisa, kidogo unakuwa unagusia mashabiki zako wanakuwa wanakupenda.” Hata hivyo Wolper japo amekiri kuwa na mchumba mpya kwa sasa lakini hayupo tayari kuweka mahusiano yake hadharani kama mwanzo alivyokuwa anafanya.....

PICHA 12: Inawezekana Daraja la ‘Kigamboni’ siku likaingia kwenye list kama hii?

Image
Mtu wangu tumeshuhudia Daraja linalounganisha Kigamboni na Kurasini likizinduliwa hivi karibuni na daraja limepewa jina la ‘Nyerere Bridge’, daraja hilo limekuwa kivutio kwa wengi ndani na hata nje ya nchi. Daraja la Nyerere ni daraja kubwa na la kisasa Afrika Mashariki na kati, uzuri na mvuto wa daraja la Mwl Nyerere ‘Kigamboni’ inawezekana ukaliingiza kwenye hii list ya haya mengine Duniani mapya yenye muonekano Mzuri? ambayo list hiyo imetolewa kupitia mtandao wa CNN April 27 2016, yatazame halafu niachie comment yako mtu wangu. Garden Bridge, (London, UK) ‘bado linaendelea kujengwa’ tayari kuna zaidi ya madaraja 30 yanayokatiza mto huo huko London lakini mradi huu mpya unaonekana kuwa kabambe zaidi. Designer Thomas Heatherwick amebuni daraja hilo kwa namna ya kufunikwa na bustani Danjlang Bridge (Talpel, Taiwan) Lucky Knot Bridge (Changsha China) daraja hili limepangwa kufunguliwa baadae mwaka huu, j

AINA ZA WASICHANA, TABIA ZAO KIMAUMBILE KATIKA MAPENZI

Image
Inasemekana wadada wana tabia tofauti katika mapenzi kulingana na maumbo ya miili yao; karibu Mtembezini uelewe kwa kwa kina vitu vinavyoweza kukusaidia kutambua tabia za watu husika. 1.Wasichana wafupi wanaongoza kwa wivu wa mapenzi na kuwajali wapenzi wao 2. Wasichana warefu huwa hawawajali wapenzi wao na hawaogopi mahusiano kuvunjia hawajui kubembeleza hata kidogo. 3. Wasichana wenye DIMPOZ, MWANYA, MATEGE MBINUKO, MAHIPS NA KITEMBE, hawa huongoza kwa kutokuwa WAAMINIFU katika mapenzi. 4. Wasichana WANENE huongoza kwa kuwa na MAPENZI YA KWELI yaani akipenda amependa kisawasawa. 5. Wasichana WEMBAMBA hawa huwa ni WABISHI sana na hawa wanaongoza kwa kutendwa! 6.Wasichana wenye NGOZI NYEUSI wanaongoza kwa KUTOA MIMBA na kupenda wanaume warefu na weupe. 7. Wasichana weupe wakiongoza kwa kuzalia nyumbani, na hawa weupe wengi wao huolewa wakiwa na watoto tayari huku wakipenda kuolewa na waarabu  kuliko wanaume weusi.

KWANINI SNURA ALITUNGA WIMBO WA CHURA?

Image
Zimepita siku tatu tangia kuachiwa kwa video ya Chura ya msanii “Snura” wakati audio ya wimbo huo ikiwa gumzo kutokana na watu wanavyojirekodi wakiucheza wimbo huo kwa staili tofauti www.mautunduyabongo.blogspot.com imefanya mahojiano na Meneja wa msanii Snura Hemed Kavu maarufu kama HK ambapo amefunguka kuhusu maana ya wimbo huo na kuhusu video hiyo ambayo inaonekana ipo nje ya maadili. “Wimbo wa Chura umelenga watu ambao wana mchezo wa kuruka ruka katika mapenzi unakuta leo upo na huyu kesho upo na yule ndio watu ambao tumewagusa kwenye wimbo wa Chura, mwanaume au mwanamke asiyetulia katika mapenzi huyo ni Chura” Akizungumzia kuwepo kwa video inayotajwa kutokuwa na maadili HK amesema video hiyo imetolewa kama bonus track na wimbo imetolewa maalum kwa mitandao ya kijamii na sio maalum kwa kuchezwa kwenye vituo mbalimbali vya habari.

UTAMU WA WANAWAKE WANENE

Image
“Lazima ujue kutofautisha kati ya msalaba na jumlisha kuna x na kuzidisha”. Si maneno yangu hayo ni maneno yake Diamond Platnumz kwenye wimbo wake wa NITAMPATA WAPI vivyo hivyo katika sifa za binadamu zipo hivyo tumetofautiana kitabia kulingana na maumbile yetu. Leo Mautundu ya bongo Mahaba imekuandalia faida za Mwanamke Mnene katika mapenzi ili upate kutambua thamani ya kila mmoja na utambue kila kitu kipo kwa makusudi na si kwa bahati mbaya; Hivyo utamu wa mwanamke mnene hutokana na vitu vifuatavyo karibu twende sawa uzitambue kwa usahihi sifa na tabia za mwanamke mnene. Wepesi wa kusamehe  Mwanamke mnene mara nyingi huwa ni mwepesi wa kusamehe pale anapokwazwa na mtu; hapendi kuweka vinyongo moyoni. Wanapenda kuomba radhi Wataalamu wa mahusiano wanasema wanawake wenye maumbo makubwa wanasifa ya kuomba radhi pale wanapokosea. Wanatulia kwa mwanaume mmoja Takwimu zinaonesha wanawake wanene sio viruka njia; mara nyingi hutulia katika mahusiano na kudu

Nay wa Mitego Aingilia Beef la Sugu na Mr Blue..Amshauri Mr Blue Nae Afute Verse za Sugu Alafu Amshirikishe Yeye.

Image
Ni siku chache zimepita tangu kutoka kwa video ya Freedom ya Sugu, video ambayo ameifanya na Director Hanscana, baada ya kutoka nyimbo hiyo kukatokea utata wa ngoma hiyo ambayo Mr blue akasema ngoma ni yake, sasa leo kupitia 255 ya Clouds FM Nay wa Mitego amefunguka kuhusiana na ngoma hiyo nakutaka kumpa idea Mr Blue. "Blue angekuwa ni mshikaji wangu ningemshauri na yeye amtoe Sugu alafu kama inawezekana aniweke mimi kwenye chorus halafu tuharibu hali ya hewa tutajuana huko mbele ya safari, halafu kama ni hela ya kuifanyia Video ngoma hii mimi nitalipa hata kwa GodFather au Hanscana‘:-Nay wa Mitego"

Ningekuwa Dhaifu Ningekuwa Nimeshajiua kwa Matusi Mtandaoni – Huddah

Image
Huddah Monroe amewataka Wakenya na wengine wanaomfahamu kumwacha aishi maisha yake. Kupitia post ndefu aliyoiweka Instagram, Huddah amedai kuwa kwa matusi anayotukanwa kila siku kwenye mitandao ya kijamii, kama angekuwa na moyo mwepesi angekuwa ameshajiua. Ameomba mara moja watu kuacha kufuatilia maisha yake na kumtukana pasipo sababu. “I, Huddah Monroe , I am known to live my life . I have no issues with anyone these days. Actually NEVER had issues with anyone unless you provoked me .HUDDAH has been the center of ridicule in this country for so many years now .People wAke up and on their Whatsapp group all they discuss is Huddah …. Creating memes about me and things I haven’t said . Thank God for my THICK SKIN, if I was a weak person I would’ve committed SUICIDE long time ago because of CYBER BULLYING…I am a grown woman now , if you have issues with me,” aliandika kwenye Instagram. “Call me , or DM and tell me what I have done to you . Or let us meet in person and

Mauzo ya Simu za iPhone yashuka

Image
Kampuni ya Apple imeripoti kushuka kwa mapato yake kwa asilimia 13 katika robo ya pili ya mwaka siku ya Jumanne huku mauzo ya iPhone yakishuka. Kampuni hiyo ya Teknolojia iliripoti kuanguka kwa mauzo yake kutoka dola bilioni 58 hadi dola bilioni 50.56 mwaka huu tangu mwaka 2003. Mauzo ya simu aina ya iPhone yalishuka kutoka milioni 61.2 mwaka 2015 hadi milioni 51.2 katika kipindi kama hicho mwaka huu. Mauzo nchini China yalishuka kwa asilimia 26,huku athari za sarafu ya dola iliozorota pia zikibainika. Hisa za Apple zilianguka kwa asilimia 8.Hisa hizo zimeanguka kwa asilimia 20 katika kipindi cha miezi 12.

Anayedaiwa Kuwa Mchepuko wa Jay Z Akanusha Kuimbwa na Beyonce Kwenye Lemonade

Image
Tangu hivi karibuni Beyoncé ‘abreak the internet’ kwa mara nyingine tena kwa kuachia album yake mpya, Lemonade, amewafanya watu wengi wamzungumzie huku wimbo ‘Sorry’ ukionekana kusababisha mjadala zaidi. Mwishoni mwa wimbo huo, Bey anasema ‘He better call Becky with the good hair.’ Baada ya mashabiki wa Beyonce kuweka connection kuwa “Becky” anaweza kuwa ni mbunifu wa mavazi, Rachel Roy baada ya kupost picha Instagram yenye maelezo ‘Good hair don’t care’, tetesi zilianza kuenea kuwa ndiye aliyechepuka na Jay Z. Na sasa mke huyo wa zamani wa rafiki yake na Jay Z, Damon Dash amelazimika kutoa maelezo kuhusiana na tetesi hizo. “I want to put the speculation and rumors to rest,” alisema kwenye maelezo yake kwa tovuti ya People. “My Instagram post was meant to be fun and lighthearted, it was misunderstood as something other than that. There is no validity to the idea that the song references me personally. There is no truth to the rumors.” Aliongeza kuwa jambo kubwa kwa

Marco Chali: Wimbo wa 'Freedom' Sio wa Mr. Blue

Image
Mr Blue analalamika kuwa Sugu ameupora wimbo wake ‘Freedom’ aliokuwa amemshirikisha kwa kutoa verse zake na kuufanyia video iliyotoka jana. Lakini katika kila malalamiko, ni vyema kusikiliza pande zote zinazohusika kwenye jambo husika ili kuupata ukweli. MJ Records walioutayarisha wimbo huo wamezungumza kuelezea mambo yalikuwaje. Producer mkuu wa studio hiyo, Marco Chali ameiambia Bongo5 kuwa beat ya wimbo huo ilitengenezwa na mdogo wake, Daxo Chali aliyetengeneza chorus yake na alimpa msanii wake Lizzy aliyeingiza. “Ngoma ilikuwa ipo tayari na ilikuwa inasubiria verse tu kadhaa halafu ilikuwa ni ngoma yake [Daxo]. Kwahiyo jamaa [Blue] akawa ameipenda tukampa akasema atamshirikisha Mr Two,” amesema Marco. Walipoifanya, Blue aliiamua kuiachia kupitia Mkito peke yake kwa maana kwamba hakuiachia ngoma rasmi. Anasema baada ya muda Sugu alimpigia simu kumuomba kuwa afanye version nyingine ya wimbo huo na aifanyie kabisa na video. Anadai alimuambia Sugu aongee na Daxo w