Utata Wazuka Kuhusu Mtu Aliyepoteza Maisha Kwenye Ajali ya Tundaman

Utata umeibuka kuhusu mtu aliyefariki kwenye ajali ya gari aliyokuwa amepanda Tundaman kutokea Njombe kuja Dar es Salaam, Jumapili hii.

Kwenye ajali hiyo, alifariki dereva aliyekuwa akiendesha aliyejulikana kwa jina la Man Katuzo. Hata hivyo imebainika kuwa, Katuzo hakuwa tu dereva, bali ndiye alikuwa bosi wa Tunda kwenye show hiyo na ndiye aliyekuwa akigharamika kwa kila kitu. Taarifa hiyo imebainika kupitia segment ya ‘Simu ya Mwisho’ inayoendeshwa na rapper Baghdad kupitia kipindi cha Papaso cha TBC FM.

Hii ni taarifa ambayo Baghdad ametutumia baada ya kuongea na ndugu wa marehemu:

Baghdad alizungumza na kaka wa marehemu ambaye ndiye msemaji wa familia juu ya kifo cha mdogo wake ambapo alithibitisha taaarifa ya kifo cha mtu mmoja ambaye hamkumtaja jina ambaye alikuwa ameketi siti ya mbele na kusema kweli Tundaman alikuwepo kwenye gari iliyopata ajali lakini hakuumia.

Aidha kaka yake aliendelea kusema ya kuwa amesikitishwa na kitendo cha wakati wa tukio Tunda aliingia kwenye gari aina ya Noah iliyokuwa kwenye msafara mmoja na gari ya marehemu na kuendelea na safari na walipofika Mikumi askari walisimamisha gari na kuikagua na kukuta bag la marehemu lenye camera 2 aina ya 5d mac 3 na lenzi tatu ambazo zililiripotiwa kupotea kwenye ajali hiyo

Kaka wa marehemu amesema Tunda hakupaswa kutokuja kumzika marehemu Man Katuzo na hajui sababu ingawa alijaribu kumpigia sana simu yake na hakupokea na kuomba kuliweka sawa kwa jamii ya kuwa simu ya marehemu kwa mara ya mwisho alipewa aishike mpaka sasa haionekani, na kama kuna lolote ambalo ni haki ya marehemu kuna yoyote alihusika kulichukua wameamua kumuachia Mungu na kusahihisha usemi wa Tundaman kuwa aliyekufa alikuwa ni dereva wake,hapana bali ndiye bosi wake ambaye alimgharamia kila kitu toka Dar kwenda kwenye show na kurejea. Marehemu Man Katuzo ameacha mke bila mtoto na amezikwa jana tar 19/4/2016 kijijini kwao Kilosa mjini Morogoro.

Kwa upande wake Tundaman alipost video inayomuonesha Katuzo enzi za uhai siku chache kabla ya mauti na kuandika: Dah nikiangalia hii video nazidi kuumia ila sisi tulikupenda ila mungu alikupenda zaidi maneno ulioniambia kuhusu familia i promise sitoyapuuza..mungu ailaze roho ya marehem musa katuzo mahali pema peponi..aamen.”

Katuzo aliyekuwa akiishi nchini Afrika Kusini, alikuwa aachie wimbo wake uitwao ‘Nguzo Saba za Sanaa’ aliomshirikisha Tundaman.

Chini ni baadhi ya picha za marehemu na mke wake:

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016