Posts

Showing posts from March, 2016

SABABU 10 ZA KWA NINI WANAUME NI VIUMBE WENYE FURAHA ZAIDI

Image
1. Majina yao ya ubini hubaki vivyo hivyo siku zote za maisha yao. 2. Maongezi yao kwenye simu huhitaji sekunde 30 tu kulizungumza jambo lililowafanya kupiga simu. 3. Safari yao ya siku 5 huwahitaji kusafiri na suruali moja tu ya jinsi. 4. Endapo rafiki yao atasahau kuwaalika katika tafrija fulani, bado wataendelea kuwa marafiki. 5. Mtindo wao mmoja wa nywele hudumu kichwani kwa miaka mingi na pengine maisha yao yote na bado wakitokea mbele za watu huwa na amani kuwa wamependeza. 6. Hata kama wanahitaji kuwafanyia shopping ndugu 25 wao hutumia dakika 25 tu na shopping ikamalizika kwa mafanikio. 7. Huwa hawakasiriki wala kujisikia vibaya wakienda kwenye tafrija na kukutana na mwanaume mwingine aliyevaa shati kama yeye, zaidi hapo urafiki huanza. 8. Wakisikia jambo hulimezea mate, hawahitaji kuwasimulia watu wengi zaidi. 9. Wakiwa wanataka kwenda kwenye mtoko mahali hawahitaji kutumia saa nzima kabatini ili kuchagua nguo ya kuvaa. 10. Wakihitaji kuwa

Diamond: Sina Tatizo na Msanii yoyote Hata Ukija Ofisini Kwangu Utakuta Nimebandika Picha ya Alikiba na Mr.blue

Image
Diamond amesema hataki kuulizwa tena kama ana bifu na msanii mwingine, amedai hana tatizo na msanii yoyote na ndio maana hata ukienda ofisini kwake utakuta ameweka picha za wasanii wote  hata ambao amekuwa akihusishwa kuwa na bifu nao. “Ukija ofisini kwangu me nna kuna picha ya blue nimembandika, kuna picha ya Juma Nature, kuna picha ya Ali , kuna picha ya Prof, Jay, kuna picha ya Ray C, kuna picha ya Q chief, TID, AY, wasanii wote wakubwa ambao anajua walianza katika huu muziki, wana mchango katika huu muziki wote me nimewaweka” Diamond Alisema  “Ofisini kwangu tu ukiingia tu reception, ukiingia tu kunasehemu nimeweka picha za wasanii wote , siwezi kuweka wote kwasababu  zisingetosha lakini kuna baadhi ya wasanii nimeweka kwasababu najua wanamchango kwenye soko la muziki wa Tanzania.” Diamond alielezea Diamond pia amesema kuwa yeye ndio huwa anahushishwa na bifu na wasanii wengine lakini yeye hana tatizo na mtu

Mwimbaji Vanessa Mdee Amfungukia Laivu Jack Patrick Aliyoko Jela....

Image
Baada ya kumkwapua Juma Mussa Mpolopoto ‘Jux’ aliyekuwa mpenzi wa modo Jacqueline Fitzpatrick ‘Jack Cliff’ kisha modo huyo kufungwa kwa msala wa madawa ya kulevya nchini China, mtoto mzuri wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee ‘V-Money’ ameibuka na kumzungumzia ‘mtalaka’ huyo wa Jux. V-Money alimfungukia modo huyo mwishoni mwa wiki iliyopita alipokuwa akifanya mahojiano maalum (exclusive) na Global TV Online ambapo pamoja na mambo mengine ya kimuziki, staa huyo anayetamba na Wimbo wa Niroge, alitumia dakika kadhaa kufafanua tuhuma zinazoelekezwa kwake kuhusiana na Jack. Awali, wanahabari wa Global TV walianza kumuuliza kama alikuwa akimfahamu Jack tangu alipokuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Jux ambapo Vanessa alijibu kuwa alikuwa hamfahamu. “Jack nilikuwa sifahamiani naye. Nilikua namjua tu ni msichana anayefanya music video na nilikuwa naona kazi zake za umodo,” alisema Vanessa kwa kujiamini. Alipoulizwa anazungumziaje kama endapo Jack atakuwa anaumia kule g

Mbunge Sugu Awachana Wasanii Kufanya Show Ulaya....Adai Sio Kigezo Kwa Music Wetu Kukua

Image
Kwenye stori tatu ya Planet Bongo ya East Africa Radio, Sugu amesema huwezi kutumia kigezo cha wasanii kufanya show nje ya Afrika yaani Ulaya, America na kwengineko kama kigezo kuwa game imekua, kwa sababu show kama hizo walishazifanya miaka zaidi ya 20 iliopita. “Huwezi kutoa credit kwa kusema wasanii wanaenda kupiga show Ulaya, Sugu, X-plastars, tumekwenda tour Europe miaka 20 iliyopita 18 au 17, kwa hiyo mimi sichukulii hiyo kama credit kama tour tulizokuwa tunapiga sisi, I apriciate hustle za kila mtu lakini sisi tulikuwa tunaenda kwenye mafestival ya dunia unapiga mbele ya mtu laki moja, ukirudi nyumbani hakuna suport kwa hiyo ili watu laki moja waliokuona kule wakupe thamani wanakuja kuangalia huko kwenu huko vipi unakuta watu wanakuzingua tu”, alisema Sugu. Sugu kwa sasa ameachia wimbo wake unaoitwa freedom, baada ya kimya kirefu kilichosababishwa na yeye kuingia kwenye siasa, mpaka kufanikiwa kutwaa jimbo la Mbeya mjini.

Soma Hapa Barua ya Binti Aliyoandika Kabla ya Kujiua Kwa Kujinyonga Kwa Kutumia Kamba Huku Longido

Image
Binti mmoja anayejulikana kwa jina la Jesca ambaye ni mfanyakazi wa Longido Mountain Lodge amekutwa amejinyonga katika hotel ya Longido Mountain Lodge na kuacha ujumbe kuwa kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote  Amesema amejinyonga kwa ridhaa yake mwenyewe.Katika ujumbe huo, ametaja majina ya watu anaowadai na kuagiza  walipe madeni yake kabla ya mwili wake kusafirishwa kwao pamoja na namba za Mama yake mzazi. "Mimi Jesca Reinald Elisante Leo tarehe 29 , 03 , 2016 nimeamua kujinyonga kwa ridhaa yangu mwenyewe hakuna mtu yeyote anayehusika na kifo changu na hizi ni namba ya Mama  yangu,0672740439. Ninao wadai Mama Diana  33,000/= John Memory card 4 GB Boss Mshahara 60,000/= wanao nidai Zai 20,000/=alipwe na ninao wadai wahakikishe wanalipa kabla sijarudishwa kwetu. NB:HAKUNA ANAYEHUSIKA NA KIFO CHANGU. Ndugu zangu nawapenda sana vitu vyangu vyote vipelekwe kwetu Jau Kwenye Kuni."

Ali Kiba na Gigy Money Mahaba Motomoto..Team Kiba Wapanick

Image
Story ya town kwa celeb wa Tz n kuwepo kwa uhusiano wa kimya kimya kati ya ali kiba na gigy money bado haijathibika japo Gigy money alipohojiwa na clouds fm kasema hajapewa ruhusa na Ali kiba kuongelea uhusiano wao kwa sasa na hawezi kuongelea kwa sasa na uko insta amewarushia kijembe mashabiki wa kiba na kuwauliza kwan kiba sio mwanaume baada ya team kiba kupanick na mapovu kuwatoka. Story hii inakuja miezi kadha baada ya Gigy kumlalamikia Jokate kumuibia Ali kiba na ikumbukwe ivi sasa Jokate hawapo kwny terms nzuri na King Kiba

Ray C Akana Kurudia Madawa ya Kulevya...Apanga Kuvishitaki Vyombo vya Habari

Image
Msanii Ray C amevijia juu vyombo vya habari vinavyoandika taarifa za uongo juu yake, kuwa amerudia kutumia madawa ya kulevya, na kuahidi safari hii atavifikisha mahakamani. Katika ukurasa wake wa instagrama Ray C ameandika ujumbe mrefu kuhusu vyombo vya habari vinavyomchafua, na kwamba wana mpango wa kukwamisha harakati zake za kupambana na madawa ya kulevya. “Hujuma hizi najua mnazifanya ili niishie njiani katika harakati za kupambana na dawa za kulevya nchini, Mimi na taasis yangu nitaendelea kusonga mbele na hakika sitakwamishwa na nyumbu kama hawa kwanza mwonekano wa picha uko wazi mimi sina nywele fupi kiasi hicho Ray C wa sasa si yule wa kipindi na enzi hizo now I'm not catalysts of drugs, hata hivyo tayari nimewasiliana na mwanasheria wangu ili niweze kuwawajibisha hawa nyumbu” aliandika Ray C. Pia Ray c amesema kwa sasa yuko kwenye maandalizi ya mwisho kuandaa nyimbo yake, japokuwa bado yuko kwenye dozi ya methadone, inayotibu uathirika w

Hizi Hapa Siri Tano za Ndoa ya Wastara Juma na Mbunge kuvunjika!

Image
Saa 24 tu tangu kupatikana kwa habari kwamba, ndoa ya staa wa sinema za Bongo, Wastara Juma aliyoifunga na Mbunge wa Jimbo la Donge, Zanzibar, Sadifa Juma imevunjika, sasa siri 5 za kuparaganyika kwa ndoa hiyo ziko mikononi mwa gazeti hili. Ndoa hiyo ilidaiwa kuvunjika rasmi Machi 21, mwaka huu baada ya kuishi kwa siku 61 tangu kufungwa kwake, Januari 8, mwaka huu huko Tabata jijini Dar. SIRI YA KWANZA Kwa mujibu wa chanzo chetu kimoja, miongoni mwa siri hizo zilizoisukuma ndoa hiyo kuvunjika ni kitendo cha Wastara kuomba kila kukicha kwamba, aachike baada ya madai kwamba, hakukuta furaha kama alivyotegemea. “Wastara alitegemea kwamba baada ya kuolewa angekuta furaha. Lakini anavyosema jambo hilo silo alilokumbana nalo ndani ya ndoa. Hiyo ni siri moja wapo, ikamfanya Wastara amuombe Mungu kila siku ili aachike,” kilisema chanzo SIRI YA PILI Chanzo kiliendelea kudai kuwa, pia Wastara aliingia kwenye ndoa hiyo huku moyo wake wote ukibaki kwa mchumba

Harmonize Atoboa Siri 'Ni Kweli Zari Hassan Ndio Aliniunganisha na Huddah Baada ya Kumtamani Kwa Muda Mrefu'

Image
Siri nje! Staa kutoka Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) anayejipenyeza kwa kasi kwenye Bongo Fleva, Rajab Abdulhan ‘Harmonize’ amekiri kuwa shemeji yake kwa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz;, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’,ndiye aliyemuunganisha na demu mkali kutoka Nairobi nchini Kenya, Huddah Monroe ‘The Boss Chick’. Akizungumza ndani ya Makao Makuu ya ofisi za gazeti hili, Bamaga- Mwenge jijini Dar, wikiendi iliyopita, Harmonize alisema kuwa kwenye maisha yake hakuwahi kuwa na ndoto ya kukutana laivu na Huddah lakini bahati hiyo aliipata akiwa nchini Afrika Kusini baada ya kukutanishwa naye na Zari. “Katika maisha yangu nilikuwa namuona tu Huddah na kumtamani ila namshukuru shemeji yangu Zari aliyenikutanisha na Huddah na kutuunganisha kuwa marafiki ambao tumekuwa tukiwasiliana utadhani tulifahamiana zaidi ya miaka hata mitano huko nyuma,” alisema Harmonize akihojiwa na Mautundu ya Bongo.

Juma Nature Adai Mshindani Wake Kwenye Muziki kwa Sasa ni Diamond

Image
Msanii mkongwe wa muziki, Juma Nature amedai msanii pekee ambaye anaweza akashindana naye kwa sasa ni Diamond. nature Akizungumza na tovuti ya Times Fm, Juma Nature ameomba wadau kuandaa tamasha ili washindanishwe. “Watu wanamtukuza sawa lakini watuweke stage moja tuone nani atakamua, unajua tuseme ukweli bongo flava sasa mimi na Diamond ndio wapinzani pekee,” alisema Juma Nature. Aliongeza, “Watu waandae pambano, na mpunga pia uwepo nioneshe na mimi nguvu yangu ilivyo mtaani,” Nature amesema anaamini muziki wake aliyokuwa anafanya zamani una nguvu kubwa kuliko huu wa wasanii wa sasa.

Wema Sepetu Atoboa Siri...Aliyekuwa Mume wa Zari Anamtongoza na Ahadi ya Kumuoa

Image
Supastaa wa Bongo, Wema Sepetu ‘madam’ ameanika siri zilizojificha nyuma ya pazia kati yake na aliyekuwa mume wa mwanamuziki nyota wa Uganda, Zarina Hassan ‘Zari’, Ivan Semwanga, kuwa anataka kumuoa. Katika mazungumzo yake exclusive na mwanahabari wetu juzi jijini Dar, Wema alianza kwa kuweka bayana kwamba, mawasiliano yake na Ivan yalianzia nchini Afrika Kusini wakati alipokwenda kikazi, Februari, mwaka huu. “Nilikwenda na Ommy Dimpoz (Faraj Nyembo). Tulikuwa na project yake lakini tulipokuwa kule, Ivan na marafiki zake walisikia kuwa mimi nipo, wakatuomba sana kupitia kwa wenyeji wetu kuwa wanataka kutuona na kutoka nao out pamoja.” “Mimi nilikuwa bize sana na kazi zangu, awali niliwaambia kuwa hatutaweza lakini baadaye walitubahatisha klabu, wakaomba kukaa na sisi, mwishoni ilibidi tuwakubalie lakini kwa masharti ya kuwa wasije wakatuzushia lolote. “Tulikubali, wakaja, tukakaa nao meza moja, tukabadilishana mawasiliano kama marafiki. Lakini baa

Chato Yatangaza Kiama cha Mapato

Image
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita, Batholomeo Manunga amewataka madiwani kuwafichua watendaji wa vijiji wanaoshirikiana na mawakala kuhujumu mapato. Akizungumza wakati wa kufungua kikao cha baraza la madiwani, Manunga amesema baadhi ya watendaji wa vijiji na kata wanahujumu mapato kwa kula njama na wazabuni. “Hatutaendelea kuvumilia hali hii, na ni jukumu letu sote kukabiliana na wote wanaohujumu mapato ya halmashauri kwa sababu bila kuongezeka hatutaweza kuwahudumia wananchi waliotuamini na kutuchagua,” amesema Manunga. Bila kutaja majina wala kata husika, mwenyekiti huyo alisema tayari halmashauri imegundua mtandao wa wanaohujumu mapato ambao wataanza kushughulikiwa baada ya uchunguzi kukamilika. Amesema watu hao wamekuwa wakiihujumu halmashauri hiyo na kuifanya ishindwe kutekeleza majukumu iliyojipangia kutokana na fedha nyingi kuishia mifukoni mwao. Manunga aliwasihi madiwani kuacha kuwaonea aibu wezi wa mali

Akina Dada Msipende Kuwadharau Vijana Mnaofanya nao Kazi Maofisini...

Image
Akina dada nipende kuwashauri kitu kimoja. Msipende kuwadharau vijana mnaofanyanao kazi ofisi moja na kuwaona wa thamani kubwa watu msiowajua hasa wa kwenye mitandao mkidhani kuwa hao ndio wana maisha bora. Ukweli ni kwamba akina dada wengi wanatabia ya kuwadharau vijana wanaoishinao wakiamini kwamba watawapata watu wenye sifa wanazozihitaji toka kwenye mitandao ya kijamii. Matokeo yake kwa sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la watoto wasiokuwa na baba au kwa jina maarufu kama watoto wa love connect, wakishazalishwa huko walikokimbilia na kuachwa ndio wanawaona wa thamani kubwa hawa waliowaacha mtaani. Ushauri kwa wadada acheni tamaa rizikeni na vijana mnao ishi nao kwenye mazingira yenu kwani wengi wao ni watu wenye nia nzuri kwenu.

Mwimbaji Rose Mhando Ashtakiwa Kwa Waziri Nape Juu ya Utapeli Anaofanya.....

Image
Msanii wa nyimbo za injili nchini, Rose Mhando, ameshtakiwa kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye, kwa kitendo cha utapeli na kushindwa kutekeleza mkataba wa kuhudhuria na kutumbuiza kwenye Tamasha la Pasaka lililofanyika jijini Mwanza licha ya kulipwa gharama zote alizotaka. Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions inayoongozwa na Alex Msama, ambayo ina mkataba naye imekuwa ikiuza na kuandaa matamasha ya msanii huyo pamoja na tamasha la Pasaka la kila mwaka, alimweleza Waziri Nnauye, mbele ya halaiki ya wananchi alipokuwa mgeni rasmi wa sherehe za tamasha hilo lililofanyika kwa mara ya kwanza jijini Mwanza na mikoa ya Kanda ya Ziwa. Msama alieleza kusikitishwa na kitendo cha Rose Mhando kuingia mitini ilihali akiwa ameingia mkataba na kulipwa gharama zote pamoja na nauli alizodai kabla ya kuanza safari kufika Geita, Mwanza na Kahama kujiunga na wasanii wenzake kwa ajili ya kutumbuiza katika tamasha hilo. “Mheshimiw

UNAJUA KAMA VYAKULA VYA MAFUTA VINA ATHIRI USINGIZI? SOMA HAPA KUJUA

Image
Wataalamu hao katika chuo kikuu cha lishe bora Colombia mjini New York alibainsha kuwa vyakula vya mafuta mengi na sukari huathiri kwa kiasi ubora wa usingizi katika matabaka yake ambapo mwanadamu hupumzikisha muili na ubongo. Utafiti huo uliendeshwa kwa kutumia watu kadhaa waliojitolea ambao umri wao ulikuwa ni miaka 35 ambapo walitumia muda wa siku 5 katika maabara ya chuo kikuu hicho.

Mambo Ambayo Wanaume Wanakosea Wakati wa Kutongoza Mwanamke

Image
1. PAPARA wanaume wengi tumekuwa na haraka sana tunapokuwa tukitaka kuaproach hali inayomfanya mwanamke akuwekee ugumu.mfano umekutana na dada mzuri mmesalimiana hapo hapo unamuomba namba yake.mjomba hata akikupa ujue utasumbuka sana kumpata coz atakufikiria sana juu ya uharaka wako. 2. KUJIFAKE wanaume wengi tumekuwa tukijipandisha au kujionyesha tofauti na hali zetu.ukiwa unaaproach jaribu kuwa real.huwezi kumwambia mdada unafanya kazi benki afu uko na techno 3. KUTOSOMA MOOD YA MWANAMKE unapomuaproach mwanamke lazma usome mood yake coz sometime unaweza kutoswa coz hujamsoma mwanamke.unamtongozaje mwanamke asubuhi?,, 4. KUMPONDA UR EX LOVE mwanamke anakuuliza kwanini uko single,unaanza kumponda ex wako kwa maneno ya kashfa hali kama hii inaweza kumtisha kisaikolojia umtongozae. 5. KULALAMIKA Unamtongoza mwanamke huku unalalamika juu ya mapenzi oooh mara sijawahi kupendwa.mjomba hapo unaonyesha udhaifu wako.UKITULIA NA KUMTONGOZA MWANAMKE BILA KUYATENDA HAYA MBNA UTAM

Nauza Bikira Yangu Kuliko Niitoe Bure Kwa Mwanaume Alafu Baadae Nijute

Image
Watu wamekuwa waongo sana , Utasikia ooohh mi ntakuoa ukinipa, siku akishapa tu anachokitaka anakula kona, mi bora tu niuze yangu, Bei poa kabisaa laki tano za kibongo..hayo ni maneno ya Msichana mmoja kutoka Kenya Alivyoandika kwenye Facebook page yake!! LAANA HII..!!By Hellen Lwasway

Baba wa Mwanamuziki Diamond Platnumz Ashinda Njaa Huku Mwanawe Akitumbua Mil 100 Ujerumani....

Image
Wakati mwanaye staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ na mwanaye Tiffah wakiteketeza kiasi cha fedha kinachokadiriwa kufikia   shilingi Mil.100 barani Ulaya walikokwenda kula bata, baba mzazi wa msanii huyo, Abdul Juma anadaiwa kushinda njaa kutokana na ugumu wa maisha, twende na Risasi Jumamosi.Baba mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Mzee Abdul Juma.Diamond na familia yake hiyo sambamba na madansa wake, waliondoka nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kwenda Frankfurt, Ujerumani ambapo pamoja na kufanya ziara ya kimuziki katika nchi tofauti balani Ulaya, staa huyo aliitumia ziara hiyo kuponda raha.Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ pamoja na mtoto wao Tiffah wakila ‘bata’ Ulaya. TUJIUNGE NA CHANZO Chanzo makini kililiambia gazeti hili mapema wiki hii kuwa, baba Diamond kwa sasa ana maisha magumu na mara n

Wema Sepetu Aingia Mkenge: Filamu yake Ya Day After Death Aliyocheza Na Van Vicker Kuishia Kabatini Kama Filamu ya Superstar Aliyomleta Omotola

Image
Wema Sepetu ni bingwa wa kutumia gharama kubwa kufanya filamu na kutengeneza kiu kubwa kwa mashabiki wake halafu then mradi unageuka kuwa kama album ya Detox ya Dr Dre, ambayo haijawahi kutoka hadi leo.June 2012: Muigizaji wa Nigeria, Omotola Jalade akiwa na Wema baada ya kuwasili kutoka Nigeria kuhudhuria uzinduzi wa filamu ya Superstar ambayo hadi leo haijatokaMiaka minne iliyopita, Wema alidai kutumia mamilioni ya shilingi kufanya filamu aliyoipa jina ‘Superstar.’ Na hata uzinduzi wake uliofanyika Hyatt Regency Hotel (Kilimanjaro) ulikuwa wa kifahari na wa aina yake. Mastaa karibu wote wa Tanzania walialikwa na kuona sehemu ya filamu hiyo.Alitisha zaidi kwa kumleta msanii nguli wa Nigeria, Omotola Jalade aliyeshuhudia uzinduzi huo. Bahati mbaya hadi leo filamu hiyo haijawahi kutoka sokoni na mrembo huyo aliamua kuifungia kabatini.Tupeleke mbele. Mwaka jana Wema alienda Ghana na kufanya filamu na staa wa huko, Van Vicker iitwayo ‘Day After Death’. Filamu hiyo ilifanyika Dec

Nay wa Mitego na Dayna Nyange Aibu Yao...Picha zao Chafu Zanaswa

Image
Hii ni aibu yao! Picha zinazomuonesha staa wa Hip Hop anayetamba na ngoma ya Shika Adabu Yako, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa katika pozi la nusu utupu na msanii wa Bongo Fleva, Aisha Nyange ‘Dayna’ zimevuja pasipo wenyewe kujua. Katika baadhi ya picha hizo, Nay anaonekana akiwa amemkumbatia Dyna huku wakiwa hawana nguo za juu,yaani Nay hana vesti wala tisheti na hata Dyna akiwa hana nguo yoyote ya kumstiri juu. Baada ya kuzidaka picha hizo gazeti hili lilivuta waya na kuwatafuta wahusika ambapo baada ya kumpata Nay na kumdadisi kama anabanjuka kimalovee na mwanadada huyo alikuwa na haya ya kusema; Dah, hapana bwana, hizo picha hatukupanga zitoke. Kuna ambazo zilipitiliza si unajua wakati wa kupiga studio zipo ambazo huwa hamzitumii sasa sijui nani alizivujisha hizo mbaya.” Baada ya kumalizana na Nay, Dyna naye alitafutwa ili kuifungukia ishu hii, ambapo baada ya kupatikana alidai zilikuwa ni picha za kwenye kava la ngoma yake ya Nitulize aliyomshirikisha Nay lakini alip

Tetesi ya Kwamba Ray C Amerudi Kwenye Matumizi ya Madawa ya Kulevya Isipuuzwe

Image
Matumizi ya Madawa ya kulevya hapa nchini yanaongezeka kwa kasi sana. Huku ikionekana wasanii ni moja kati ya waathirika wa kubwa wa janga hili. Tumeona hivi karibuni rapa mkongwe Chidi Benz jinsi alivyothorofika kutokana na matumizi ya Madawa ya kulevya.Kupitia mitandao ya kijamii kumekuwa na tetesi kwamba Ray C amerudi katika matumizi ya madawa ya kulevya ingawa mara kadhaa amekuwa akikanusha taarifa hizo.Waswahili wana msemo mashuhuri usemao ‘Lisemwalo lipo’ kwa nini asitajwe msanii wengine, na mara nyingi wasanii wote ambao hutumia Madawa ya kulevya, uanza kwa kukataa hadi pale akapozidiwa ndipo anaweka wazi. Tumeshuhudia kwa Chidi Benz, Ray C, Q Chief na wengine .Februari mwaka huu, Ray C alikanusha vikali taarifa ya kwamba amerudi kwenye matumizi ya madawa ya kulevya , “Hata siju moja sikawahi pata msaada wowote kutoka kwenu japo kunichangia nauli tu ya kuja kwenye dawa kila siku hakuna hata anaenisaidia huu mwaka wa tatu bado naendelea kunywa dawa na ni kila siku ya mungu sik

Umaarufu wamfanya Harmonize aishi kwa shida

Image
Msanii kutoka lebo ya WCB Harmonize, ametoa siri ya maisha ya wasanii ambao wako chini ya lebo hiyo, ambayo inawafanya kuepuka mambo mengi ikiwemo skendo chafu, huku akidai kuwa wanafuata nyayo za bosi wao Diamond Platnums.Harmonize ameongea hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa East Africa Radio, na kusema kuwa wao kama WCB hawana kawaida ya kwenda club kutokana na kubanwa na majukumu, na pia hata bosi wao ambao ni mfano mzuri kwao, hana kawaida ya kwenda sehemu kama hizo. “Labda nizungumze kitu kimoja, WCB sio mimi tu hata wasanii wengine ambao watatoka WCB kuna life style ambayo watafuata, lakini mimi kama mimi sipajui club kabisa, sijawahi kwenda club sitokagi, kwa sababu pale ofisini kuna studio studio mle mle ndani, kuna vyumba ambavyo ukirekodi ukichoka unakaa unarefresh mind, kuna game station mnakaa mnacheza game, alafu pia kuna vyumba vya kuishi mule mule, muda wenyewe wa kutoka unakosa, alafu pia ukizingatia CEO mwenyewe wa WCB hana hizo mambo za kwenda club, so sisi tun

KWANINI WANAWAKE HAWAPENDI KUTOKA KIMAPENZI NA WANAUME WAFUPI? SABABU 4 ZIKO HAPA

Image
 Utafiti nili usoma siku moja kuhusu wanaume wafupi, na walisema wanaume wafupi wana mapenzi ya kweli na ya dhati kuliko wanaume warefu, kitu ambacho siwezi bisha sababu, wanawake wengi huwa hawapendi kutoka na wanaume wafupi kwahiyo inawachukua sana muda kupata mwenza na lazima wawapende na wawape mapenzi ya kweli wanawake zao ili wasiwaache  kwa sababu wanawake wengi wanapenda mwanaume  warefu na wengi wana mvuto kuliko wafupi. Wanawake wengi wanapenda kutoka na wanaume ambao wamewazidi urefu hata kidogo, kuliko kuwa na mwanaume ambaye ni mfupi kuliko wao,wengi wanasema hii inaleta picha mbaya au muonekano mbaya wakiwa wanaongozana wanaita (not Marching), lakini kuna sifa nyingine za wanaume wafupi wanawake wengi wanasema zinawakera kama, Wivu Inasemekana wanaume wafupi wana wivu wa kupindukia na sio kama wanaume wengine warefu hawana wivu ila wivu wao unapitiliza kiasi cha kukera kwani wivu ukizidi sana ni kero katika mapenzi. Wanaume wengi wafupi wana sifa sana, kiasi cha kuke

WANAWAKE WENGI HUFIKIRI WANAUME WOTE WANA TABIA HIZI

Image
Hakuna  maana moja ya kumuelezea mwanaume, ila kwa aliye mwanaume nadhani anaelewa nini maana ya kuitwa mwanaume, mara nyingi wanawake huwa wanaonekana wao ndio wanaonewa sana na wanaume na ni vigumu sana kujua manyanyaso ya wanaume sababu wengi huwa hawayaongelei, wanawake wengi huwaongelea wanaume kwa ujumla yaani kuwafananisha wote katika kundi moja. lakini kuna mtu na mtu kila mtu ana tabia zake na wanaume wana tofautiana, sina maana ya  kutetea haki za wanaume ila kuna fikira potofu kuhusu wanaume ambazo watu wanatakiwa kuzitoa akilini. Mwanaume halii. Mwanaume akionekana analia ataitwa dhaifu, ama hajakuwa bado mtoto, lakini ukweli ni kwamba hata wanaume wana hisia wana umia na wana mioyo kama wanawake, wao sio maroboti  japokuwa inachukuliwa kuwa mwanaume anayaeweza kuvumilia maumivu ndio jasiri bila kujua sio kila anaye lia kwa machozi ni mnyonge. Kuna usemi wa mwandishi Malorie Blackman alisema “Boys don’t cry, but men do.”  katika kitabu chake cha  Boys Don’t Cry. Wanaume

Dudubaya Afunguka...Watu Mfano wa Chid Benz Hawatakiwi Kusaidiwa Kabisa...Kifo Anakitaka Mwenyewe

Image
Baada ya rapa Chidi Benz kuomba msaada ili asaidiwe kuirudisha afya yake ambayo imethorofika kutokana na matumizi ya Madawa ya kulevyana na baadae kusaidiwa na Babu Tale kwa kupelekwa rehab. Wadau mbalimbali pamoja na wasanii wenzake walimpongeza Babutale lakini Dudu Baya amedai hakupenda rapa huyo asaidiwe.DuduAkizungumza na Bongo5 Jumamosi hii, Dudu amedai rapa huyo hakuwa tayari kusaidiwa ndio maana baada ya kusaidiwa anataka kujipangia baadhi ya mambo.“Watu mfano wa Chidi Benz hawatakiwi kusaidiwa, niwakuachwa wafe na wazikwe. Kwanza ni waongo, ukikutana nao utasikia naumwa au nimefiwa, utampa msaada, mwisho wa siku anaenda kujidunga. Misaada kama hii inatufanya majina yetu kuwekwa kataka orodha ya wauaji (killers),” alisema Dudu. Aliongeza, “Babutale na wenzake walipomfisha Chidi Benz rehab kwanza alianza kuweka masharti yake kituoni, mara hawezi kushauriwa na mtu ambaye hajawahi kutumia sumu hiyo (unga). Hapo ndipo nilipogundua amebebwa kinguvu bila yeye kuwa tayari kupona. Ni

Maoni: Hofu yangu Kuhusu Label ya Wasafi, Diamond, Harmonize na Raymond ni Kama ‘Mtu Mmoja’

Image
Makala imeandikwa na Wynjones Kinye (Mhadhiri chuo kikuu cha SAUT)Naappreciate sana juhudi za Diamond katika kuunyanyua muziki wa Tanzania kwa kuibua vipaji vipya kama Harmonize, Raymond na watakaofuata kama wapo.Ni dhahiri kuwa kwa hili la kusimamia vijana wawili tu kiasi kikubwa cha fedha kimetumika na kinaendelea kutumika hasa ukizingatia kuwa Diamond tayari ni mtu sensitive kwenye quality ya product, na tunajua kuwa quality ni gharama kubwa siku hizi kama sio siku zote. Diamond amethubutu kuwekeza, kibiashara tunategemea return katika kila unachofanya ‘kibiashara’ hivyo ni muhimu sana kufikiria vitu vingi vya kuifanikisha biashara ukiachana na mtaji. Hata kama una mtaji mkubwa na fedha za ziada kuuendeleza mradi bado failure iko pale kama hutotazama vitu vingine kwa kina.Licha ya nguvu nyingi anayoweka Diamond kwenye muziki wa vijana wake ‘publicity na video nzuri’ bado mimi nina hofu ya kufanikiwa kwake kuwafikisha vijana wake hawa chini ya label yake. Nilivumilia kulisema hili

Mashabiki Wakerwa na Kauli Hii ya Zari, Wadai Amewakejeli Maskini

Image
Labda ukweli unauma.. Kwamba wengi tunatamani sana maisha mazuri anayoishi Diamond na mchumba wake, Zari the Bosslady. Wapo wanaoishia kutamani na kumuomba Mungu nao waje kuwa na maisha hayo, wengine hushukuru na hufurahi tu kwa kile walichonacho ama tumeseme wameridhika na kidogo wanachopata.Lakini wapo ambao hushindwa kujizuia kupata wivu na kuwachukia tu watu wenye mafanikio – wa kuitwa haters. Hayo ni majaribu makubwa waliyonayo mastaa duniani. Lakini sio mara zote huvumilia matusi na kejeli wanazozipata kwenye mitandao ya kijamii.Wakati Zari akiendelea kula raha Ulaya na mchumba wake Diamond, ameendelea kutupiwa vijembe na watu kuwa hawajali tena wanae watatu aliowaacha Afrika Kusini, kwamba kila siku kiguu na njia na Diamond. Hilo limemkera, na ameamua kulijibu.Staa huyo amepost picha hiyo juu na tafsiri yake kwa maneno hayo ni:Watoto wangu wameniuliza, kwanini kila mtu amechukia? Nimewaambia tuna vitu ambavyo hawana. Wakati mnachukua, mimi naenda mall, kumwaga fedha. N

Kuvaa Nusu Utupu Natangaza Brand- Vanessa Mdee

Image
Msanii wa muziki wa bogno fleva ambaye anafanya poa katika anga za kimataifa Vanesa mdee , amefunguka sababu ya yeye kupenda kuvaa nguo za nusu utupu.Akiwa kwenye kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa na East Africa Radio na EATV, Vanessa Mdee amesema anapenda kuvaa mavazi hayo ambayo hayakubaliki kwa jamii, kwa sababu anatangaza brand yake, na hatimaye impe dili la matangazo kwa wabunifu wa mavazi. “Ukweli ni huu, wasanii for a long time in the past, wasanii wa kitanzania hawajajua na kutambua brand yao, mi brand yangu mi nataka ndani ya miaka miwili napigiwa simu na Balmain, na Lui V, nataka dersigners wakubwa wa dunia wanitumie kutangaza bidhaa yao kwa sababu wanaamini nina brand yangu kubwa na zinaendana, so nna malengo , na if im gonna offend any body im sory”, alisema Vanessa Mdee. Vanessa Mdee ambaye kwa sasa ameachia video yake mpya ya Kaniroge, amesema ana mipnago ya kufika na kutambulika dunia nzima katika kazi zake za muziki, kama alivyochora ramani ya dunia kweny

Je Linah Sanga Amewahi Kutoa Rushwa ya Ngono? Majibu yako Hapa

Kipindi cha Enews kinachorushwa na East Africa Television kilitaka kufahamu kama kuna ukweli wasanii hao wa kike huhonga ngono ili wafanyiwe kazi nzuri kwenye hizo kampuni kubwa, Linah Sanga ambaye hata yeye amefanikiwa kufanya videos na waongozaji wakubwa wa video barani Afrika akiwepo Godfather alikuwa na haya ya kusema. "Sijui kama ipo hivyo sababu mimi kama msanii wa kike sijawahi kufanya kitu kama hicho, kwa hiyo sidhani kama hicho kitu ni cha kweli kwa sababu ukifuatilia kwa wasanii wakubwa wa kike ambao tumeweza kufanya kazi na madirectors wakubwa kama God Father na wengine ni mimi, Vanessa, labda na Aika kwa sasa hivi ambao tayari tumeshatoa kazi zetu, kwa hiyo sidhani kama hicho kitu ni kweli kwa sababu tunafanya kazi na kazi zinalipa ndiyo maana tunaweza kufanya kazi na watayarishaji wakubwa kama hivyo". Alisema Linah Sanga.

Basi la Princess Muro Laacha Njia na Kuingia Kwenye Kituo cha Mabasi ya Mwendo Kasi

Image
Basi la kampuni ya Princess Muro lapata ajali baada ya kupoteza mwelekeo na kuingia kituo cha Magari ya Mwendo kasi Kimara jijini Dar es Salaam.Endelea kufuatilia taarifa zetu tutakujuza kwa kina taarifa hii.

Diamond Platnumz aliwahi kumtoa damu Chid Benz,Maneno ya Bab Tale yako hapa..

Image
Meneja wa Diamond Platnumz ‘Bab Tale’ ameweka wazi kuwa Diamond Platnums alishawahi kumsaidia Chidi Benzi kuacha madawa, kwa kwenda kumtoa damu na kumuwekea damu safi, lakini jambo hilo lilikuwa la siri ndio maana aliweza kurudia.Tale anasema “Diamond alimshamtoa Chidi damu, kutoa ile yenye madawa, lakini alirudia unajua Chid anaacha na kurudia, sasa labda ndio maana ilikuwa rahisi kwa yeye kurudi kwa sababu ilikuwa siri, Damond siku hiyo alishinda hospitali kutwa nzima, akimtoa Chidi damu“. Kwa sasa Chid Benzi amepelekwa Rehab bagamoyo baada ya kurudia matumizi ya madawa ya kulevya, na kumuathiri kwa kiasi kikubwa, na ameahidi kuacha matumizi ya madawa hayo.

Msanii wa Sauti Sol ‘Delvin’ ahusishwa kimapenzi na mpwa wa rais Uhuru Kenyatta.

Image
Msanii wa Sauti Sol ‘Delvin’ ameripotiwa kuwa na mahusiano na mpwa wa rais Uhuru Kenyatta anayefahamika kama Kavi Pratt.Delvin hakuwa na aibu kuweka mahusiano yao wazi kiasi cha kuweka picha wakiwa pamoja, na alipoulizwa alijibu “You can’t deny the power of attraction and a kiss does not necessarily mean that there is more. It is good to allow people to show affection.” akimaanisha “Huwezi kataa nguvu ya mvuto wa mtu na busu halina maana kuna kitu zaidi, ni vizuri kuruhusu watu kuonyesha wanakukubli” Kavi alishuka kupata swali hio na kuomba muda zaidi kabla hajajibu.

Fumanizi mbaka kifo hapo hapo..

Image
Mume na mke kutoka RUVUMA majina yao hayaku tambuliwa haraka chazo ni mke alimuaga mume wake anaenda kwenye mkutano wa injili MBEYA. Mume bila kinyongo akamruhusu ila akasoma mchezo yule alipo sepa mume wake akapanda basi la nyuma akawa anamfukuzia walipo fika MBEYA stand huyo mke akaenda kyela na mshikaji akamfuata hivyo mke akawa na mpenzi mwingine kwenye hiyo guest naye akachukua chumba hapo hapo bila mke wake kujua. Yule mke akiwa na mpenzi wake chumba kingine kumbe mume Wake kalala pale pale usiku mume halali akawagongea wakijua kuwa muhudumu jamaa kaingia na tindikali yenye mchanganyiko mzuri wa acid akawamwagia wote na yeye mwenyewe mule chumbani na wote wakafa.

Peter wa P Square abadilisha jina la kisanii, Jina jipya liko hapa.

Image
Msanii wa kundi la P-Square ‘Peters Okoye’ aliyetoa wimbo wake wa “Look Into My Eyes” amebadlisha jina kutoka kwenye Peter Okoye na kuanza kujiita ‘Mr. P’  kama ishara ya kuanza kufanya kazi kama solo artist. Peter ametambulisha jina hili kwneye club moja huko Abuja alipofanya show bila pacha wake Paul Okoye. Pia Peter anashow nyingine mnamo April 7, 2016 huko Dubai.

Polisi nchini Marekani wavamia nyumba ya Davido,Sababu na alivyojitetea,viko hapa.

Image
Kwa mujibu wa Africa Facts Zone, polisi nchini Marekani wamevamia nyumba ya Davido iliyopo mjini Atlanta, Georgia wakimtuhumu kuwa ni mtu anayekusanya na kusafisha pesa za mambo ya kihalifu. Polisi walifanya hivyo baad aya kuchunguza maisha ya kifahari anayoishi Davido bila kujua kipato chake kinatoka wapi kwenye eneo hilo analoishi. Davido alitumia ukweli kwa kuwaambia yeyeni staa wa muziki kutoka Nigeria na kuwaonyesha Channel yake ya Youtube inavyotazamwa na zaidi ya watu milioni 100.

Diamond Platnumz akisema kitu kilichomfanya Kanye West kutaka kupiga naye picha.

Image
Baada ya picha ya staa wa bongo fleva Diamond Platnumz akiwa na Hip Hop staa kutoka Marekani, Kanye West kusamba pamekuwa na maswali mengi ya Ilikuaje mpaka picha hii ikapigwa?  Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo, kinachoruka kupitia EA Radio, Diamond alisema, “Nilipokuwa airport pale Los Angeles tunasubiri kuchukua mabegi yetu, nilisikia mtu akisema ninaweza kupiga picha viatu vyako? Kwakuwa alikuwa ameinama sikuweza kumtambua lakini alipoinuka nikashangaa kumuona ni brother Kanye West. Nilimuomba tupige picha kwanza halafu vingine vitaendelea.” Kuhusu collabo D alisema“Tumuombe Mungu mambo yaendelee vizuri kama tulivyopanga, kuna kitu kizuri kinaweza kikatokea kati yetu"