Posts

Showing posts from July, 2016

Nilivyofanya Bonge la Sherehe Baada ya Mke Wangu Kufukuzwa Kazi

Image
Huyu mke nilimuoa akiwa hana kitu, kwa bahati alitafutiwa kazi na ndugu yake kwenye kampuni moja ya simu akawa analipwa kama milioni 3 kwa mwezi fasheni na yeye yeye na fasheni vipodozi kila aina,handbag na nywele za laki mbili ndio mshahara wake ukawa unaishia huko mimi mshahara wangu hauzidi laki sita,nilifanyishwa vituko vyote ndani ya nyumba ,manyanyaso yote ,hapiki hafui,hafanyi chochote ndoa ikawa inaelekea kuvunjika. Nikaenda mahakamani kuprocess talaka wakasema mpaka nianzie baraza la usuluhishi la kata au kanisani,nikaamua kwenda kanisa tulilofungia ndoa tukaitwa kwa Baba Paroko for hearing sijui mediation sijui arbitration sijui mie nikatinga kwa bajaj ya kukodi nimepaukaaa yeye akaja na RAV4 . Baba Paroko alivyotusikiliza akaaniita pembeni akasema kijana hapa nadhani hata tukiomba na kukariri mistari yote ya biblia plus mapambio yote ndoa yako haitarudi kama mwanzo pambana utafute hela ,huyu ni mchaga katumwa pesa mjini Nilisali sana nikasugua g

Malaika:Sitaki Tena Mpenzi wa Bongo

Image
Diana Exavery ’Malaika’ MSANII wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Diana Exavery ’Malaika’ amefunguka kuwa kwa sasa hataki tena mpenzi Bongo badala yake akitokea mtu kutoka nje ya nchi, yuko radhi kuwa naye. Akizungumza na Risasi Vibes, Malaika ambaye hivi karibuni alimwagana na mpenzi wake Mbongo, anayefahamika kwa jina moja la Dadi, alisema wanaume wengi wa Tanzania ni pasua kichwa, jambo linalomfanya ajaribu nje kuona “Sitaki tena mpenzi wa hapa kwa sasa, maana wengi wana tabia zinazofanana, lakini akitokea mtu wa nje poa, naweza kuwa naye,” alisema msanii huyo.

MWIMBAJI Baraka Da Prince Ala Shavu Nono..Sasa Anakula Sahani Moja na Ali Kiba na Lady Jay Dee

Image
Hitmaker wa Siwezi, Barakah Da Prince amesainishwa mkataba wa usimamizi na kampuni ya Rockastar4000. Ameungana na Alikiba na Lady Jaydee kuwa msanii wa tatu kuwa chini ya uongozi huo. Na kwa sasa muimbaji huyo atakuwa akijulikana kama ‘Barakah The Prince.’ Kwenye maelezo yake, CEO na mwanzilishi wa label hiyo, Jandre Louw amedai kufurahishwa kumsaini muimbaji huyo wa Mwanza na kumwelezea kama mwenye kipaji cha hali ya juu. Akiwa chini ya label hiyo, Barakah ataanza kuandaa album yake ya kwanza itakayotoka mwaka 2017. Muimbaji huyo amejipatia umaarufu kwa nyimbo zake kama Siachani Nawe, Nivumilie na Siwezi.

MADAM Rita Afunguka Kuhusu Ukimya wa Top 5 ya Washindi wa Bongo Star Search 2015

Image
Najua nina watu wangu ambao watakuwa na maswali mengi juu ya kuhusu wale Top 5 wa Bongo Star Search 2015, sasa basi Ayo TV imemtafuta Jaji Madam Rita kufafanua zaidi. ‘Sisi tuna mkataba na uongozi wakina Babu Tale yaani Tip Top Connection wao kuna vitu wanafanya kwasasa maandalizi yao, kwahiyo kuna vitu vinapikwa kutoka kwa wasanii hao watano unajua watu wanahisi msanii akitoka Bongo Star Search anajulikana siku hiyo hiyo hapana kuna watu wanachukua miaka mitano au miaka mikumi ndio wanakuja kujulikana’- Madam Rita
Image
Kwenye zile stori za kwenye mitandao ambazo zimefatiliwa sana ni pamoja na hii ya Ommy Dimpoz kukutana na Wayne Rooney mchezaji wa Manchester United wakiwa Ibiza na kisha kupiga picha ambayo imebeba vitu vingi tusivyovifahamu na pengine tulihitaji kufahamu. Picha ambayo imepigwa na Dimpoz ni picha ya video ambayo wanaonekana wanazungumza kitu lakini sauti ya video hiyo imezimwa (mute) so wakati tunasubiri Ommy Dimpoz mwenyewe atuambie walichokuwa wanazungumza ninayo hiyo video mtu wangu ambayo Ommy Dimpoz kapost kwenye akaunti yake ya Instagram. Kwenye post zake Ommy Dimpoz ameonekana akila raha sehemu mbalimbali za Ibiza,mahali ambako mastaa wengi wa Dunian hutembelea kwa ajili ya mapumziko.
Image
Kibano! Staa wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amejikuta kwenye mikono ya sheria na kuswekwa lupango baada ya  kumtukana shosti yake, Miss Kinondoni 2009, Stella Mbuge. Kwa mujibu wa mtoa ubuyu wetu makini, Kabula alitaitiwa na polisi usiku wa Jumatano iliyopita mara baada ya kutendo kosa hilo walipokuwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar wakitazama mechi kati ya Yanga na TP Mazembe ya DR Congo. “Walipishana kauli kule uwanjani, si unajua Kabula ni Yanga damu, sasa nahisi alishindwa kustahimili utani wa Stella ndipo akamporomoshea matusi ambayo yalimfanya mwenzake akimbilie polisi. “Alikwenda kushtaki Polisi Kijitonyama (Mabatini), akapewa polisi na kwenda kumkamata Kabula ambaye wakati huo alikuwa kwenye sherehe ya mtoto wa Esha Buheti. Wakamtia ndani hadi kesho yake (Jumatano) walipomtoa kwa dhamana,” kilisema chanzo chetu. Baada ya kunasa ubuyu huo, Jumatano iliyopita, Risasi Jumamosi lilimtafuta Kabula ili kumsikia anazungumziaje ub
Image
Msanii mkongwe wa muziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ amefunguka kwa kusema kuwa hataki tena kukaa kimya kwa muda mrefu bila kuachia kazi. Muimbaji huyo ambaye ameachia wimbo ‘Sawa na Wao’ hivi karibuni, amekiambia kipindi cha East Africa Breakfast kinachoruka East Africa Radio kuwa anachofanya ni kutoa kazi moja moja kutoka katika albamu yake mpya iitwayo’Women’. “Unajua mimi nina marafiki mbalimbali wa rika zote, wapo walionizidi sana umri, wapo nalingana nao na wengine ni wadogo zangu kabisa hivyo muda mwingi napotoka nao au kujichanganya nao ndipo nikapata wazo la wimbo huu ‘Sawa na wao’ kwani binadamu tunatofautiana. Saizi nimeamua kila baada ya miezi mitatu nitakuwa natoa kazi moja kutoka kwenye album yangu hiyo ya ‘Woman’,” alisema Lady Jaydee. Lady Jaydee amesema wazo la wimbo ‘Sawa na Wao’ ambao ameuachia hivi karibuni alilipata kutokana na maisha ya watu wake wa karibu ambao amekuwa akiishi nao katika maisha ya kila siku.

Ajifungua Kwenye Korido Baada ya Kukosa Huduma kwa Wauguzi

Image
Mjamzito mmoja, Magreth Charles (22), mkazi wa Kata ya Lyabukande Wilaya ya Shinyanga amejifungulia kwenye korido la Kituo cha Afya cha Lyabukande baada ya kukosa huduma kutoka kwa wauguzi. Mjamzito huyo alilazimika kujifungulia kwenye korido kutokana na wauguzi katika kituo hicho kugoma kutoa msaada wakidai wako kwenye mapumziko na kumtaka aende sehemu nyingine. Mama mkwe wa mjamzito huyo, Rachel Mpanda alisema walifika kituoni hapo wakitokea kijiji cha Kizungu jirani na kituo hicho na walielezwa na mtu waliyemkuta kuwa wauguzi wako mapumzikoni, hivyo hakutakuwa na huduma yeyote. “Baada ya muda kidogo tukiwa tunatafuta namna ya kwenda kituo kingine, mwari wangu alianza kusukuma mtoto, hivyo nikaamua kuomba msaada kwa wapitanjia ili wamsaidie ajifungue, alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume,” alisema Mpanda. Diwani wa kata hiyo, Joseph Misiri alisema tukio la mwanamke huyo kujifungua kwenye korido si la kwanza na kwamba kuna mwanamke mwingine alikosa