Diamond platnumz na Qeen Darling Baba ni Baba tu, Baba Yenu Kawaomba Msamaha Msameheni Kabla Hamjachelewa.



Nimeona interview ya Clouds TV na Mzee Platnumz, kweli jamaa kachoka. Huyu ni Baba yake na mwanamuziki matata nchini Diamond Platnumz.
Kama alikukosea wewe na mama yako, mbona ameshasema mumsamehe? Bila ya yeye Diamond asingekuwa alivyo sasa. Hivyo inatakiwa Diamond awe na moyo mkubwa wa kusamehe mtu ambaye ameshaomba kusamehewa. Binadamu tuna mapungufu na ni ujasiri ulioje kukubali kuwa umekosa na kuomba kusamehewa.

Diamond ni kioo cha jamii, uwe na moyo wa kusamehe. Pia kwa Queen Darlin, Baba yenu kawaomba msamaha wote.
Msaidieni Baba Yenu ana Hali Mbaya

9 comments:

  1. Akifanikiwa mwanao, wakati mama anahustle peke yake hakuwa wako nyooo, hayo ni matokeo ya wanaume kukwepa majukumu yao!
    Reply
  2. sio ttz la kina mama km angekua karibu na wanawe na kutimiza wajibu km baba yasingemkuta haya usimlaumu mama hata ww baba yk angekutelekeza ukapata shida na mama yk ungeujua uchungu alipotelekeza familia alijua wanakula nn wanalala wapi wanavaa nini anagutuka saivi km yy ni baba
    Reply
  3. Bado atabaki kuwa Baba yake aliyemleta duniani. Alishatimiza wajibu wake kwa Allah, kuomba msamaha kwa kujua aliikosea familia. Tunaishi kiimani hata kama Ni kuabudu miti. Kwa wewe mwislam mwenzangu kasome Quraan(17:23)" And your lord has decreed that you worship none but him. And that you be dutiful to your parents. If one of them or both of them attain old age in your life, say not to them a word of disrespect, nor shout at them but address them in terms of honour". Kazi kwako unayeamini uwepo wa Mungu na anayotuelekeza. Napenda mwandishi unapomtetea mzazi. Kwa Mungu Una fungu lako. Japo Kuna wanaodhani Ni sahihi. Mzazi atabaki kuwa mzazi
    Reply
  4. Hakuna hurumaaaa uwiii mm ndo najua adha ya kutelekezwa weeeee..baba anakwambia kwanza we sio mwanangu unaomba ada anakwambia kajiuze kama mama yako upate ada ya shule kweliii??haya bado anakwambia we unafir****w kama mama yako kweli baba huyu unabaki unajiuliza ni baba yangu kweli au baba anakutukana matusi mazito tena na mamayako juu aisee hapana mi baba yangu sitaki kumuona tulivyohangaika kusoma unaambiwa kauze mkun**d upate ada jamni acheni haya mambo yasikie tu shout out kwa wababa wote wanaojua majukumu yao mi mume wangu ndo amekuwa baba rafiki mpenzi na mume yani vyote kwa anavyonifariji..baba yetu tumemuachia Mungu ataulipia
    Reply
  5. We daimond umekua kama cio muislam rudia tena kusoma nini wazazi wawili katika uislam halafu ndio ufanye upumbavu wako me ni fan wako but kwa hilo im not with u bro.
    Reply
  6. huyu mzee ni msanii tuu hana lolote anajifanya kurudi kwa domo coz ana mafanikio
    katika wa baba wavivu na wahuni huyu yumo ni wale masharobaro wa zamani akipata pesa ananunua nguo na madem wamshobokee uswahilini starehe kibao atamaisha yake kashidwa kuyatengeneza
    watoto wote kashindwa kuwahudumia huyu baba ziro kweli
    ata ningekuwa mimi domo namfungia vioo tuu
    kwanza bado ana nguvu zake afanye kazi aache shobo
    Reply
  7. Usimpe wazo Hilo kwa baba ake mzazi
    Reply
  8. msimlaumu mzee Abduli kasema ukweli alimfumania bi Sandra ndo maana akaondoka pia alimsaidia Dai kuwa staa pale aliambiwa aende kwa sangoma. sasa washakuwa maarufu wamemsahau ndo maana anaanza kutoa siri zote.
    Reply
  9. Wakati anawatosa hizo dini zilikua wapi. Saiz mtt kafanikiwa ndo kelele nyingi. Msamaha watoto walishamsamehe anachotaka uyo mze ni mshko na kick tu. Afu na ww mwandish acha kutetea usilolijua uyo baba kaeleza mabaya ya sandra mbona yake hasemi. Halafu ugomvi wao ndo awatose watoto. Anayemtetea huyu mbaba hayajamfika yakikukuta uwezi mtetea aende zake kule. Mi namunga mkono dai hakuna cha baba nibaba apa tena akae kimya ampotezee tu. Eti nilimshauri kwenda kwa mganga, kwa hiyo unataka malipo ya kwenda kwa mganga ata soni hana. Yani yy ndo alichochangia kwenye mafanikio ya mwanae. Ujinga mtupu.
    Reply

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016