Ufisadi Mkubwa Wabainika Wilaya ya Ilala..Aliyekuwa Meya Jerry Slaa Aushishwa Kushindwa Kuzibiti Akiwa Meya



KUNA mambo mengine ni ya aibu hata kutamka hadharani. Chama chenu mnakinyonga wenyewe kwa mikono yenu kisha mnatafuta wachawi.

Hebu fikiria, uongozi wa Meya wa Ilala ndio kwanza imeanza kazi chini Charles Kuyeka (Ukawa). Wamefanya ukaguzi wa ndani wa mahesabu. Yani hata hawajamaliza tayari wameibui uvundo huu hapa.

"Tumebaini mshahara uliopitishwa na Manispaa kulipa Mgambo ni 280,000/- kwa mwezi na mikataba ya ni miezi mitatu mitatu lakini wamekuwa wakilipwa Kati ya Sh 50,000/- hadi 80,000/- ilhali kwenye vitabu inabaki 280,000/-" Mungu wangu!

Kuyeko anaongeza: "baya zaidi agizo na hitaji la Manispaa ni Mgambo 150 lakini inaonesha walikuwa wakishaajiriwa 150 hupunguzwa kijanja na kubaki 100 lakini vitabuni ni 150". My God! Kweli Jerry Silaa haya yamefanyika ukiwa Meya wa Ilala na hukuyaona?

Kumbe ndio maana mgambo wakimkamata Mamalishe cha kwanza wanawahi masufuria ya ubwabwa na nyama! Kumbe kuna hamuwalipi ipasavyo!! Ninahisi machozi kunitoka. Why you look soo smart haya ulibariki. Mbona mnakidhalilisha CCM namna hii?

Kumbe hata hizi figisu figisu za Umeya ni kutaka kuficha maukoko haya yanayonuka. Na huo ni ukaguzi wa awali tu.

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016