Nuh Mziwanda – Shilole Kanifanya Nishindwe Kununua Hata Feni Amwomba Radhi Mama yake...Kwa lipi?

 
Msanii wa bongo fleva Nuh Mziwanda amefunguka na kusema kuwa mpenzi wake wa zamani Shilole alikuwa hataki yeye amiliki kitu chochote kwa kuhofia kwamba anaweza kumkimbia iwapo atafanikiwa.

Msanii huyo pia amemwomba radhi mama yake na ndugu zake ambao kila siku walikuwa wanamsihi ajipange lakini yeye alikuwa anawachukulia poa na kusema amejifunza mengi.

Nuh alifunguka hayo wakati akilelezea kitu gani kilimfanya asijipange vizuri kimaisha.Msanii huyo alifunguka na kusema
“Ni kweli nilikuwa naishi kwa mwanamke wangu na alikuwa hataki ninunue hata feni..wazazi wangu walikuwa wakiniimiza kujipanga,leo nimeyaona.Namwomba msahamaha mama yangu,ndugu zangu marafiki zangu walikuwa wakinipa ushauri mimi nikawa naona nimepata kumbe nimepatikana” alifunguka Nuh na kusema kwa sasa maisha yake yamekuwa mazuri hata mashabiki zake wanamkubali zaidi.

Post a Comment


Emoticon

Comments

Popular posts from this blog

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 4 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 3 Exam Answers 100% 2016

IT Essentials (ITE v6.0) Chapter 2 Exam Answers 100% 2016