Mahsusi kwa watu wanaotarajia kuanzisha mahusiano thabiti na yenye
malengo pamoja na wale ambao tayari wamo ndani ya mahusiano ya aina
hiyo imekuandalia vitu vya kuzingatia karibu twende sawa.
KWA WATARAJIWA
1.Usidanganyike na muonekano wa nje au yale maongezi ya mwanzo, Kila mtu hua mstaarabu siku za mwanzo hata wale ambao sio.
2.Usikimbilie kutangaza nia haraka.
Siku zote ni rahisi mtu kua
muwazi kwa rafiki yake kuliko kwa mtu ambae anajua anataka mahusiano nae
kwa hofu ya kumpoteza.Tumieni muda wakutosha kufahamiana kama marafiki
kabla hamjajiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi.
3.Uliza maswali kuhusu vitu ambavyo ni muhimu sana kwako.
Kwa mfano kama ni mtu wa familia au sio taka kujua mawazo yake
kuhusu watoto hii itaepusha migongano isiyo ya lazima hapo baadae.
4.Penda kujua malengo yake ya baadae.
Hii itakuwezesha kugundua ni mtu wa aina gani kama ni mpenda maendeleo,mtu wa starehe tu n.k.
5.Kuwa muwazi.
Hii inakwenda kwa pande zote kuna vitu ambavyo ukimwambia mtu ni vidogo sana ila ukificha vinakua kwa vile tu ulifanya siri.
6.Hakikisha uwezo wenu wa kuelewa unaendana.
Hapa siongelei darasa ila mnavyokua sambamba kwenye maongezi ya kawaida tu yasiyo hitaji degree.
7.Onyesha Misimamo yako hata kama unaona ni migumu kueleweka.
Ni vizuri mtu akikubali/taka
kujiingiza kwenye mahusiano na wewe awe akijua atakua na mtu wa aina
gani kama hupendi nguo fupi,mwanamke/mwanaume mnywaji wa pombe, mvuta
sigara n.k sio unasubiri mpaka muwe pamoja ndo muanze kuzozana.
8.Hakikisha kuna vitu Mnavyo Shabihiana.
Ni muhimu mkiwa na vitu
mnavyoweza kufanya pamoja iwe ni kuangalia movie ama kutembea nyakati za
jioni inasaidia kuimarisha ukaribu wenu kuliko kila mtu kwenda na njia
yake.
WAKATI Mwisho Mwampamba aliposhiriki kwa mara ya kwanza Shindano la Big Brother miaka ile ya mwanzo wa 2000, Wabongo wengi hawakuwahi kufikiri kama ni kitu ambacho kingeweza kuwasaidia vijana wetu, hata pale dau kubwa la mshindi lilipotangazwa. Wengi walitazama zaidi katika maadili, kwa sababu kulikuwa na mambo mengi ambayo kwa utamaduni wetu, hayakustahili kuoneshwa katika televisheni kama yalivyokuwa yakifanyika. Lakini taratibu wakajikuta wanaliona shindano hilo kuwa la kawaida, lenye ‘kuburudisha’ hasa baada ya ushindi wa Richard mwaka ule wa 2007. Leo hii, vijana wawili wa Kitanzania tayari wameweka kibindoni jumla ya dola 400,000 kutoka shindano hilo, kwani Richard alichukua dola laki moja alipotwaa ushindi na Idriss Sultan, aliyeibuka namba moja mwaka jana, kwa pesa ya madafu, ana kama milioni 500 hivi! Sasa Idriss amekuwa kijana maarufu sana katika jamii yetu, akiwa ngazi moja y...
Dalili za Mke anayetoka nje ya ndoa: 1) Anatembea na vidonge vya majira kwenye mkoba wake, wakati mume amefanyiwa Vasectomy (Kufunga kizazi kwa mwanaume) 2) Anakuwa na namba ya siri ya simu ambayo mume haijui 3) Anatumia muda mwingi anapokwenda sokoni au kufanya manunuzi ya wiki 4) Anajinunulia nguo za gharama zikiwemo nguo za ndani bila kumshirikisha mume 5) Anakuwa akitegemea zaidi ushauri kutoka nje kwa watu wengine zaidi ya mumewe 6) Anaacha kuvaa pete ya ndoa bila sababu 7) Anapopigiwa simu akiwa karibu na mumewe anaizima au kwenda kupokelea nje 8) Anakuwa hajali tena mambo ya familia na hujiamulia mambo yake mwenyewe 9) Ni rahisi sana kusema ‘nipe talaka yangu’ inapotokea kutofautiana hata kwa jambo dogo. 10) Dharau na kejeli kwa mume hujionyesha waziwazi Dalili za mume anayetoka nje ya ndoa: 1) Unakuta Condom kwenye mkoba wake au kwenye gari lake wakati umefunga kizazi au unatumia vidonge vya majira. 2) Anapunguza au anaacha kabisa kuwa outing na fa...
Mtindi unaorodheshwa kuwa miongoni mwa vyakula bora kutokana na kuwa na virutubisho vingi vya aina mbalimbali ambavyo vina faida nyingi katika mwili wa binadamu. Vikitajwa kwa uchache virutubisho hivyo, imethibitika kuwa mtindi ni chanzo kizuri cha ‘Calcium’, ‘Phosphorus’, ‘Riboflavin (vitamin B2), ‘Iodine’, ‘vitamin B12’, ‘Pantothenic acid (vitamin B5) ‘Zinc’, ‘Potassium’ na ‘Molybdenum’. Mbali ya virutubisho hivyo, ndani ya mtindi kuna ‘bakteria hai’ ambao ni muhimu kiafya katika mwili. HUREFUSHA MAISHA Utafiti unaonesha kuwa unywaji wa mtindi mara kwa mara, hasa katika kundi la wazee, uwezo wa mwili wa kupambana na magonjwa mbalimbali umeonesha kuongezeka na kufanya mfumo wa kinga ya mwili kuwa imara zaidi. Katika utafiti mmoja, walichaguliwa wazee 162 ambao walipewa utaratibu wa kunywa mtindi na maziwa zaidi ya mara 3 kwa wiki na kufuatiliwa maendeleo yao kwa muda wa miaka mitano. Baadaye utafiti huo ulionesha kuwa idadi ya vifo vya wazee hao ilipungua kwa...
Comments
Post a Comment