Mama Wema Sepetu Asema Kuna Wakati Anapigana na watu Kumtetea Wema


Mama yake Wema Sepetu, Mariam Sepetu amefunguka na kueleza jinsi anavyoumizwa na stori za uongo kuhusu mwanae ambazo zimekuwa zikiandikwa katika magazeti ya udaku.
wema

Akizungumza katika kipindi cha Clouds E cha Clouds TV Alhamisi hii, Bi Mariam amesema amekuwa akigombana mara kadhaa na baadhi na viongozi wa magazeti ya udaku kuhusu stori za uongo.

“Naumia sana kama mzazi, Wema alishaambiwa kwamba ana maradhi ya ngono, kama mzazi najisikia vibaya sana,” alisema Mama Wema. “Mimi nikishasikia hivyo nawafuata watu wa magazeti, nagombana nao sana. Kuna wakati nampigia Wema namuuliza jana ulitoka, anasema hajatoka, ukiwa kama mzazi inauma sana, wao wanauza magazeti kutokana na stori za uongo za mwanangu,”

Aliongeza, “Nimeshapigana na watu kuhusu Wema, wanakuja nyumbani wanaanza kuongea maneno maneno ambayo hayaeleweki,”

Comments

Popular posts from this blog

Idriss Sultan Una Uhakika Gani Kama Mimba ya Wema Sepetu ni Yako?

Nitajuaje ama Mke au Mume Wangu Anatoka Nje ya Ndoa? Mambo Gani Yanaweza Yakaonyesha?

Hizi Hapa Faida za Kunywa Maziwa Mgando/Mtindi Katika Mwili wa Binadamu